5.4.3 Plasenta kama kichungi

Mojawapo ya majukumu ya plasenta ni kutumika kama kichungi. Plasenta huruhusu chembe zenye manufaa kwa fetasi, kama vile oksijeni na virutubishi, kupita kutoka kwenye mfumo wa damu ya mama hadi wa fetasi. Hata hivyo, plasenta pia hujaribu kuzuia vitu vyenye madhara kupita. Kwa mfano, plasenta huruhusu protini na baadhi ya kemikali kubwa katika damu kupita, zikiwemo antibodi, ambazo ni kemikali zinazoundwa mwilini mwa mama ili kukumbana na viini vinavyosababisha maambukizi, kama vile bakteria. Kuachilia antibodi kuvuka kupitia kwenye plasenta hadi fetasi ni jambo la muhimu ili kukinga fetasi, na baadaye mtoto mzawa kutokana na viini hivi vinavyosababisha maambukizi.

Hata hivyo, plasenta haiwezi kuzuia alkoholi, baadhi ya dawa na virusi kuvuka hadi katika fetasi. Vitu hivi vinaweza kusababisha hitilafu za kuzaliwa, kama vile meno kugeuka rangi, hitilafu ya mifupa na kuharibika kwa ubongo. Ni muhimu kumshauri mama mjamzito kukomesha matumizi ya dawa zenye madhara na kuepukana na kemikali hatari. Ulijifunza mengi kuhusu maswala ya uhamasisho wa kiafya katika utunzaji wa wajawazito katika Kipindi cha 14.

5.4.2 Mzunguko wa damu kwenye plasenta

5.4.4 Usanisi wa homoni katika plasenta