Muhtasari wa Kipindi cha 5

Katika Kipindi cha 5 ulijifunza:

  1. Utungisho ni kuungana kwa seli ya uzazi ya kiume na za kike, mbegu ya kiume na ova, katika mishipa ya falopio.
  2. Mbegu za kiume zinaweza kusalia hai katika mfumo wa uzazi wa mwanamke kwa kipindi cha saa 72. Ova husalia hai kwa saa 12 hadi 24 tu. Ili utungusho ufanyike, ni sharti mbegu ya kiume ishushwe ukeni kwa kipindi kisichozidi siku tatu kabla ya ovulesheni, na kisichozidi saa 24 baada ya ovulesheni.
  3. Baada ya utungisho, seli hujigawa na kuunda hatua za embrio inayokua, zikiwemo morula (bonge la mviringo la seli) kisha blastosisti (mviringo wa seli wenye mwanya).
  4. Embrio hushuka kutoka katika falopio hadi uterasi kwa siku 5 -7.
  5. Embrio hupandikizwa katika endomitriamu (pembezoni) ya uterasi. Ikiwa itapandikizwa kwenye falopio, mimba ya kiektopi hutokea, na ni hatari sana kwa mwanamke.
  6. Eneo la trofoblasti ya blastosisti hupenya kwenye endomitriamu, na michomozo inayoitwa vili hutoa kemikali zinazoyeyusha mishipa ya damu ya mama. Damu ya mama hulowesha mishipa ya damu ya fetasi katika plasenta, kisha virutubishi, oksijeni na takamwili hubadilishanwa kati ya mama na fetasi.
  7. Damu ya mama na ya fetasi haichanganyiki katika plasenta.
  8. Plasenta hutenda kazi kama eneo la kusafirishia, kichungi cha kutenganisha dutu muhimu na hatari, na kiungo cha kutolesha homoni.

5.4.4 Usanisi wa homoni katika plasenta

Maswali ya Kujitatmini ya Kipindi cha 5