6.1.1 Iliamu

Iliamu hutamkwa kama ‘il-a-mu’

Sehemu kuu ya pelvisi imeundwa kwa mifupa miwili, kila mojawapo ikiitwa iliamu - mfupa mmoja katika kila upande wa uti wa mgongo (au safu ya uti) kisha kupindika kuelekea upande wa mbele wa mwili. Ukiweka mkono wako kwenye kiuno kimoja, utakuwa umeshika kilele cha iliamu, ambao ni mpaka wa juu wa iliamu katika upande huo ulioshika. Katika sehemu ya mbele ya kilele cha iliamu, unaweza kushika na kuhisi chomozo la kimfupa liitwalo uti wa juu wa mbele wa iliamu (’chomozo’ ni kitu kinachobenuka nje, kama vile mlima au nundu).

  • Je, istilahi ya kimaelekezo ‘juu’ na ‘mbele’ yanatufahamisha nini kuhusu nafasi ya nyuti za iliamu? (Iwapo hukumbuki, rejelea Jedwali 3.1 katika Kipindi cha 3.)

  • ‘Mbele’ humaanisha kuwa nyuti za iliamu ziko katika sehemu ya mbele ya mwili. ‘Juu’ inaashiria kuwa nyuti hizi ziko juu ya sehemu kuu ya iliamu katika kila upande.

    Mwisho wa jibu

6.1 Pelvisi ya mwanamke iliyo ya kimfupa

6.1.2 Iskiamu