6.1.2 Iskiamu

Iskiamu ndiyo sehemu ya chini nene ya pelvisi iliyoundwa kwa mifupa miwili iliyoungana - mfupa mmoja katika kila upande. Mwanamke anapokuwa katika leba, mshuko wa kichwa cha fetasi inaposhukia katika njia ya uzazi hukadiriwa kwa kulinganishwa na nyuti za iskiamu, ambazo ni chomozo za iskiamu zinazoelekea ndani katika kila upande. Nyuti za iskiamu ni ndogo zaidi na za umbo la duara zaidi katika pelvisi ya mwanamke kushinda ile ya mwanaume. Katika Moduli ya Leba na Utunzaji wa wakati wa Kuzaa, utajifunza jinsi ya kuhisi nyuti za iskiamu ili kukuwezesha kukadiria jinsi kichwa cha fetasi kilivyoshuka katika njia ya uzazi.

Iskiamu hutamkwa kama ‘is-ki-amu’

6.1.3 Mifupa ya kinena na simfisisi ya kinena