6.1.4 Sakramu

Sakramu hutamkwa kama ‘sa-kra-mu’. Kokisiksi hutamkwa kama ‘koki siksi’.

Sakramu ni mfupa mrefu, wenye umbo la kabari ulio nyuma ya pelvisi, ambao una vetebra tano zilizoshikana (mifupa midogo inayounda safu ya uti wa mgongo au uti wa mgongo). Chini ya sakramu ni chomozo la kimfupa linalofanana na mkia liitwalo kokisiksi. Mpaka wa juu wa vetebra ya kwanza katika sakramu huchomoza na kuelekea upande wa mbele ya mwili. Chomozo hili ni promontori ya sakramu - ambayo ni sehemu muhimu katika leba.

6.1.3 Mifupa ya kinena na simfisisi ya kinena

6.2 Njia ya pelvisi