6.2 Njia ya pelvisi

Uwazi mgumu wa duara uliofunikwa na mfupa wa kinena upande wa mbele na iskiamu wa nyuma, huitwa njia ya pelvisi - uwazi wa mifupa ambao mtoto hupitia. Njia hii ina umbo lililopindika kwa sababu ya tofauti ya ukubwa kati ya mipaka ya mbele na ya nyuma ya uwazi ulioachwa na mifupa ya pelvisi. Unaweza kuiona njia hii kutoka mtazamo wa upande kwenye Mchoro 6.2.

Mchoro 6.2 Njia ya pelvisi ikitazamwa kutoka upande mmoja, huku mwili ukielekea upande wa kushoto.

6.2.1 Ukubwa na umbo la pelvisi