6.2.3 Kitokezi cha pelvisi

Kitokezi cha pelvisi kimeundwa kwa mpaka wa chini wa mifupa ya kinena upande wa mbele na mpaka wa chini wa sakramu upande wa nyuma. Nyuti za iskiamu zimechomoza kuelekea pande zote mbili. Mchoro 6.4 kinaonyesha ukubwa wa nafasi ambayo ni sharti fetasi kupitia inapotoka katika pelvisi la mama. Unapotazama Mchoro 6.4, chukulia kuwa wewe ni mkunga anayetazama juu katika njia ya uzazi huku ukingonjea fetasi ichomoze kichwa.

Mchoro 6.4 Kipenyo cha kiingilizi cha pelvisi kikiangaliwa kutoka upande wa chini.
  • Je, unatambua nini unapolinganisha ukubwa wa kiingilizi cha pelvisi (Mchoro 6.3) na kitokezi cha pelvisi (Mchoro 6.4)? Ni gani nyembamba zaidi kati ya milango hii miwili?

  • Kipenyo chembamba zaidi cha kuiwezesha fetasi kupitia ni kitokezi cha pelvisi ambacho kina upana wa sentimita 11 pekee katika pelvisi ya mwanamke ya wastani.

    Mwisho wa jibu

Ni vigumu kutambua kutoka Mchoro 6.3 na 6.4, lakini ni sharti fetasi izunguke ili iweze kupitia katika njia ya pelvisi. Hii ni kwa sababu kiingilizi cha pelvisi ni sentimita 13 kwa upana ilhali kitokezi cha pelvisi ni sentimita 11 pekee kwa upana. Ili iweze kutoshea katika kitokezi cha pelvisi katika sehemu pana zaidi (sentimita 12.5 kutoka juu hadi chini), ni sharti fetasi izunguke ili iweze ’kutanguliza' kichwa chake kwenye upande ule mpana zaidi wa njia ya pelvisi katika kila sehemu wakati inapopita. Fuvu ndiyo sehemu iliyo kubwa zaidi ya fetasi, hivyo kichwa cha fetasi huzunguka kwanza, kisha mabega, halafu sehemu ya mwili iliyobakia kutanguliza. Utajifunza haya yote katika Moduli ya Utunzaji wa Leba na Kuzaa. Kwanza, hebu tuutazame vyema muundo wa fuvu la fetasi.

6.2.2 Kiingilizi cha pelvisi

6.3 Fuvu la fetasi