6.3.2 Sucha

Sucha ni viunga vilivyo katikati ya mifupa ya fuvu. Katika fetasi, sucha hizi zinaweza 'kubonyeka' kidogo chini ya shinikizo kwenye kichwa cha mtoto anaposhukia kwenye njia ya uzazi. Mwanzoni mwa utotoni, sucha hizi huwa gumu na mifupa ya fuvu haiwezi kusonga ikilinganishwa na kila moja wake, jinsi inavyosonga ingawa kwa kiasi kidogo katika fetasi au mtoto mzawa. Katika masomo ya ukunga, ni jambo la kidesturi kufunza majina na maeneo ya mifupa hii. Unaweza kutambua pembenukta ya kichwa cha mtoto 'anapotanguliza' katika njia ya uzazi kwa kuhisi zilipo sucha kuu kwa vipimo vya vidole vyako. Unaweza kuona mahali zilipo sucha katika fuvu la fetasi katika Mchoro 6.6, na pia vipenyo vyake katika ncha mbili.

Sucha hutamkwa kama ‘su-cha’.

Mchoro 6.6 Maeneo na sehemu muhimu kwenye fuvu la fetasi zikielekea upande wa kushoto, kama zinavyoonekana kutoka juu. Makinika kuhusu vipenyo wastani vilivyoonyeshwa kwa rangi nyekundu.
  • Sucha la lamdoidi huunda muungano kati ya mfupa wa oksipitasi na mfupa wa paji.

Lamdoidi hutamkwa kama ‘lam doidi’. Sagita ni ‘sa-ji-ta’ ilhali korona ni ‘ko-ro-na’.

  • Sucha ya sajita huunganisha mifupa miwili ya parieta.
  • Sucha ya korona huunganisha mfupa wa paji na mifupa miwili ya parieta.
  • Sucha ya paji huunganisha mifupa yote miwili ya paji.
  • Unatambua nini kuhusu vipenyo vilivyopeanwa katika Mchoro 6.6, ukilinganisha na ukubwa wa njia ya pelvisi (Mchoro 6.3 na 6.4)?

  • Katika sehemu pana zaidi, fuvu la fetasi lina upana wa sentimita 9.5 (kwa wastani). Hii ni sentimita 3.5 chache zaidi kuliko kipenyo kipana zaidi cha kiingilizi cha pelvisi na sentimita 1.5 chache zaidi kuliko kipenyo kipana zaidi cha kitokezi cha pelvisi.

    Mwisho wa jibu

Hii ni kumaanisha, ikiwa pelvisi ya mama na fuvu la fetasi ni vya ukubwa wa wastani, kuna nafasi ya kutosha ya kichwa cha mtoto kupitia katika njia ya pelvisi ikiwa kichwa kitazunguka ili kutokea katika eneo kubwa zaidi la pelvisi.

6.3.1 Mifupa ya fuvu la fetasi

6.3.3 Fontaneli