6.3.3 Fontaneli

Fontaneli ni nafasi inayoundwa sucha mbili au zaidi zinapoungana. Fontaneli huwa imefunikwa kwa tando nene na ngozi ya kichwa cha mtoto, huku ikiukinga ubongo ulio chini yake ili usipate mathara kutoka nje. Kutambua fontaneli mbili kubwa juu ya fuvu la fetasi husaidia kujua pembenukta ambayo kichwa cha mtoto kinatanguzia wakati wa leba na kuzaa. Fontaneli zinaonyeshwa katika Mchoro 6.5 na 6.6. Fontaneli hizi ni:

  • Fontaneli ya mbele (pia inayojulikana kama bregma) ni nafasi yenye umbo la almasi inayoelekea katika sehemu ya mbele ya kichwa cha mtoto katika muungano wa sucha za sajita, korona na paji. Fontaneli hii ni laini sana na unaweza kuhisi mpigo wa moyo wa fetasi kwa kuviweka vidole vyako taratibu juu ya fontaneli hizi. Ngozi iliyo juu ya fontaneli inaweza kuonekana 'ikidunda' katika mtoto mzawa au mtoto mchanga.
  • Fontaneli ya nyuma (au lamda) ina umbo la pembetatu, na inapatikana kuelekea nyuma ya fuvu la fetasi. Fontaneli hii imeundwa kufuatia muungano wa lamdoidi na sucha za sajita.

6.3.4 Maeneo na sehemu muhimu katika fuvu la fetasi