6.3.4 Maeneo na sehemu muhimu katika fuvu la fetasi

Vielelezo 6.5 na 6.6 vinakuwezesha kutambua maeneo maalum na sehemu muhimu katika fuvu la fetasi, ambazo zina umuhimu maalum katika utunzaji wa kiukunga. Hii ni kwa sababu zinaweza kuunda sehemu maarufu kama sehemu tangulizi ya fetasi - ambayo ni sehemu inayoelekea chini ya njia ya uzazi.

  • Veteksi ni eneo la katikati ya fontenali ya mbele, mifupa miwili ya parieta na fontenali ya nyuma. Utangulizi wa veteksi hutokea wakati sehemu hii ya fuvu la fetasi inatangulia. Hii ndiyo njia ya kawaida na iliyo salama zaidi ya utangulizi wakati wa kuzaa kwa njia ya uke.
  • Paji ni eneo la fuvu linalotandaza kutoka fontaneli ya mbele hadi kwenye mpaka wa juu ya macho. Utangulizi wa paji ni hatari kubwa kwa mama na mtoto.
  • Uso hutandaza kutoka tuta la juu ya macho hadi kwenye pua na kidevu (kitaya cha chini). Utangulizi wa uso pia ni hatari kubwa kwa mama na mtoto.
  • Osiputi ni eneo la katikati mwa msingi wa fuvu na fontenali ya nyuma. Ni jambo lisilo la kawaida na hatari sana kwa osiputi kuwa sehemu inayotanguliza.

Utakaposoma moduli inayofuatia ya Utunzaji wa Leba na Kuzaa, utajifunza kuhusu tangulizi za aina nyingine ikiwemo 'kutanguliza matako' (kichwa cha mtoto kinapoelekea juu na miguu yake au matako ndiyo sehemu inayotangulia), na 'bega' kwanza.

Kwa kuwa umejua sehemu kuu maumbile ya mfumo wa uzazi mwanamke, pelvisi ya mwanamke na fuvu la fetasi, sasa tuende katika Kipindi cha 7 ili tuweze kutazama mabadiliko makuu ya kifiziolojia yanayotokea katika mwili wa mwanamke wakati yu mjamzito.

Muhtasari wa Kipindi cha 6