Muhtasari wa Kipindi cha 6

Katika Kipindi cha 6 umejifunza kwamba:

  1. Mifupa ya pelvisi ni pamoja na iliamu, isikiamu, mifupa ya kinena, na sakramu.
  2. Ukubwa na umbo la pelvisi linaweza kuathiri urahisi au ugumu wa leba na kuzaa. Pelvisi pana hurahisisha kuzaa kuliko pelvisa nyembamba, ambayo inaweza kuzuia kushuka kwa mtoto katika njia ya kuzaa.
  3. Sehemu mahususi ambazo ni muhimu za maumbile ya pelvisi hutumika mara nyingi kukadiria jinsi mtoto alivyshuka wakati wa leba na kuzaa. Sehemu mbili zilizo muhimu zaidi ni nyuti za iskiamu na promontari ya iskiamu, ambayo inaweza kuhisika kwa vidole wakati wa kuchunguza uke.
  4. Kiingilizi cha pelvisi ni nafasi ambayo kichwa cha mtoto huingilia pelvisi. Mlango huu wa pelvisi ni mkubwa kuliko kitokezi cha pelvisi ambapo kichwa cha mtoto hutokea. Mtoto hulazimika kuzunguka anapopitia kwenye njia ya pelvisi, ili kuhakikisha amepata kipenyo kikubwa cha kiingilizi na kitokezi cha pelvisi.
  5. Fuvu la kichwa limeundwa kwa mifupa mingi iliyounganishwa na viunga viitwavyo sucha. Katika fetasi na mtoto mzawa, nafasi ziitwazo fontaneli ziko kati ya baadhi ya mifupa ya fuvu iliyo juu ya kichwa cha mtoto. Nafasi ya sucha na fontaneli inaweza kubainisha kuhusu pembenukta ya kutokeza kwa kichwa cha mtoto wakati wa leba na kuzaa.
  6. Kutanguliza veteksi (ambapo sehemu ya juu ya kichwa cha mtoto hutangulia) ni hali ya kawaida na salama zaidi katika uzazi wa kawaida wa kupitia uke. Hali zingine za kutanguliza huwa hatari zaidi kwa mama na mtoto.

6.3.4 Maeneo na sehemu muhimu katika fuvu la fetasi

Maswali ya Kujitathmini (MK) ya Kipindi cha 6