Maswali ya Kujitathmini (MK) ya Kipindi cha 6

Kwa kuwa sasa umekamilisha Kipindi hiki, jibu maswali yafuatayo ili kubaini jinsi ulivyotimiza Malengo ya Masomo ya Kipindi hiki. Andika majibu yako katika shajara yako ya masomo na uyajadili na mkufunzi wako katika Mkutano Saidizi wa Somo unaofuata. Unaweza kudhibitisha majibu yako ukilinganisha na vidokezo ulivyoandika katika Maswali ya Kujitathmini yaliyo mwishoni mwa Moduli hii.

Swali la Kujitathmini 6.1 (linatathmini Malengo ya Somo 6.1, 6.2 na 6.3)

Linganisha kila jina la kimaumbile na maelezo yaliyo sahihi.

Using the following two lists, match each numbered item with the correct letter.

  1. Mfupa wa nyonga katika pelvisi

  2. Jozi la mifupa linalounda sehemu ya mbele ya fuvu

  3. Viunga vilivyo kati ya mifupa ya parieta katika fuvu la fetasi.

  4. Vetebra zilizoungana za mgongo zilizo nyuma ya pelvisi

  5. Sehemu ya juu ya fuvu la fetasi katikati ya fontaneli mbili

  • a.Iliamu

  • b.Veteksi

  • c.Sakramu

  • d.Mifupa ya paji

  • e.Sucha wa sajita

The correct answers are:
  • 1 = a
  • 2 = d
  • 3 = e
  • 4 = c
  • 5 = b

Swali la Kujitathmini 6.2 (linatathmini Malengo ya Somo 6.1, 6.2 na 6.3)

Ni elezo lipi ambalo si kweli?? Katika kila kauli, eleza ni kwa nini sio sahihi.

  • A.Mifupa ya pelvisi ya mwanamke ni pana na bapa kuzidi ile ya mwanaume.
  • B.Kiingilizi cha pelvisi ni kidogo kuzidi kitokezi.
  • C.Ncha ya iliamu ni sehemu muhimu ya maumbile ya kubaini jinsi fetasi inavyoshukia ukeni.
  • D.Sucha katika fuvu la fetasi ni viunga vigumu na thabiti ambavyo hushikamanisha mifupa ya fuvu.
  • E.Mpwito wa mtoto mzawa unaweza kuonekana ikidunda katika fontaneli ya mbele.

Answer

A ni kweli Mifupa ya pelvisi ya mwanamke ni pana na bapa zaida ya ile ya mwanaume.

B si kweli. Kiingilizi cha pelvisi ni kipana (wala si chembamba) kuliko kitokezi.

C si kweli. Kilele cha iliamu ni chomozo lililo katika sehemu ya mbele ya mfupa wa kiuno. Kilele cha iliamu si sehemu muhimu ya kubaini jinsi fetasi inavyoshukia ukeni.

D si kweli. Sucha katika fuvu la kichwa cha fetasi ’hubonyea' kidogo kufuatia shinikizo la uke, hivyo mifupa ya fuvu la kichwa inaweza kuchezacheza kidogo. Jambo hili hufanya kichwa cha mtoto kupitia katika pelvisi ya mama kwa urahisi.

E ni kweli. Mpwito wa mtoto mzawa unaweza kuonekana ukidunda katika fontaneli ya mbele.

Mwisho wa jibu

Swali la Kujitathmini 6.3 (linatathmini Malengo ya Somo 6.1, 6.2 na 6.3)

Orodhesha sifa 4 zinazoweza kuwa za pelvisi na/au fuvu la fetasi ambazo zinaweza kutatiza leba au kuzaa.

Answer

Sifa za pelvisi na/au fuvu la fetasi zinazoweza kutatiza leba au kuzaa ni pamoja na (unafaa kutaja nne tu):

  • Pelvisi nyembamba au iliyoumbuka
  • Ukuaji wa tishu usio wa kawaida katika uwasi wa pelvisi
  • Fuvu kubwa la fetasi.
  • Fetasi kutanguliza paji, uso, matako au mabega.
  • Fetasi ambayo haiwezi kutanguliza sehemu pana zaidi la fuvu lake katika sehemu pana zaidi ya kiingilizi cha pelvisi, kisha kuzunguka na kufanya vivyo hivyo katika kitokezi.

Mwisho wa jibu

Muhtasari wa Kipindi cha 6