7.9 Mabadiliko katika matiti

Katika vipindi vya kwanza vya ujauzito, matiti yanaweza kuwa na hisia za kujaa au kuchoma, huku yakiongezeka kwa ukubwa pindi ujauzito unavyoendelea. Areola (duara nyeusi ya ngozi yenye rangi) inayoizunguka chuchu huwa nyeusi zaidi huku kipenyo chake kikiongezeka. Tezi za Montgomery (vijinundu vilivyo katika areola) huongezeka kwa ukubwa na kuonekana kuchomoza. Mishipa ya damu ya sehemu ya juu ya titi inaweza kuanza kuonekana kufuatia ongezeko la kuzunguka kwa damu. Mishipa hii inaweza kuyapa matiti yangi ya waridi.

Kufikia wiki ya 16 (wakati wa simesta ya pili), matiti huanza kutoa dang’a. Hii ndiyo dutu inayotangulia maziwa ya titi. Dang’a ni dutu ya manjano inayotoka katika chuchu ambayo huwa nene zaidi pindi ujauzito unavyoendelea. Dang’a ina kiasi cha juu sana cha protini na huwa na antibodi (protini maalum zinazotolewa na mfumo wa kingamwili ya mama) ambazo husaidia kumkinga mtoto mzawa kutokana na maambukizi. Mwisho wa ujauzito unapokaribia, chuchu zinaweza kutoa dang’a nyingi kiasi cha kufanya majimaji kwenye nguo ya mama. Mhakikishie mama kuwa jambo hili ni la kawaida na ni ishara nzuri. Baada ya mtoto kuzaliwa, dang’a hutolewa kwa takriban siku tatu za kwanza, kabla ya maziwa halisi kuanza kutiririka. Hakikisha kuwa mama anamyonyesha mtoto kwa dang’a ili apate virutubishi vyote na antibodi anazohitaji.

Katika Kipindi cha 8, utakumbana tena na baadhi ya dalili za mabadiliko haya ya kifisiolojia ya ujauzito, ambapo utajifunza jinsi ya kutambua iwapo mwanamke ni mjamzito, na jinsi ya kukusanya habari kuhusu ’historia yake ya ujauzito’.

7.8.4 Tezi za jasho

Muhtasari wa Kipindi cha 7