Muhtasari wa Kipindi cha 7

Katika Kipindi cha 7, ulijifunza yafuatayo:

  1. Vile vile, estrojeni na projesteroni ni homoni kuu katika kipindi chote cha ujauzito.
  2. Miongoni mwa athari zingine, viwango vya juu vya projesteroni husababisha ukubwa wa baadhi ya viungo vya ndani ya mwili kuongezeka, ikiwa ni pamoja na uterasi, ili iweze kubeba mtoto aliyehitimu muhula wote wa ujauzito.
  3. Ongezeko la uzito linalotarajiwa kwa mwanamke mwenye afya njema, aliye na mimba ya hali ya wastani na aliyebeba mtoto mmoja ni kama ifuatayo:
  4. Mwili huhitaji kiasi kikubwa cha damu inayozunguka ili kuwepo kwa damu ya ziada itakayopitia katika plasenta ili lishe na oksijeni ifikishwe kwenye fetasi.
  5. Ongezeko la kiasi cha damu huzidi ongezeko la seli nyekundu za damu, hivyo zinachujulika katika kiasi hiki kikubwa cha plazma ya damu, jambo linalosababisha anemia. Hii ni sababu moja inayofanya nyongeza ya ayoni mwilini kuwa muhimu sana wakati wa ujauzito.
  6. Shinikizo la chini la damu ni kawaida hususani katika kipindi cha mwanzo wa ujauzito. Jambo hili linaweza kupelekea kizunguzungu na hata kipindi kifupi cha kukosa ufahamu.
  7. Upungufu wa kurejea kwa damu moyoni ni jambo linaloweza kupelekea edema - kufura kwa miguu na nyayo kufuatia viowevu kukusanyika humu.
  8. Wakati wa ujauzito, wanawake wengi hukosa hewa ya kutosha kwa sababu mtoto anayekua husukuma mapafu ya mama hivyo ana nafasi ndogo zaidi ya kupumua. Mwanamke huyu pia anaweza kukumbwa na matatizo ya umeng’enyaji kwa sababu fumbatio lake husukumwa juu zaidi.
  9. Wakati wa ujauzito, misuli ya pembezo za mfumo wa tumbo na utumbo hulegea kidogo, kisha kima ambacho chakula husafirishwa tumboni hupungua kidogo. Jambo hili hupelekea virutubishi kufyonzwa kwa kiwango cha juu zaidi katika damu ya mama, jambo ambalo hunufaisha fetasi. Hata hivyo, mama huyu anaweza pia kupatwa na kichefuchefu au matatizo ya umeng’enyaji.
  10. Haja ya kukojoa kila mara ni jambo la kawaida, hasa katika mwezi wa kwanza na wa mwisho wa ujauzito. Hii ni kwa sababu uterasi inayokua husukuma kibofu. Kibofu hujaa upesi zaidi wakati wa usiku kwa sababu kiowevu (edema) kinachokusanyika miguuni wakati wa mchana hufyonzwa tena.
  11. Mabadiliko katika homoni za mwanamke na kupanuka kwa kimaumbile kwa matiti na fumbatio linalokua ni mambo yanayoweza kusababisha alama za kuvutika katika ngozi inayofukia maeneno haya wakati wa ujauzito. Mabadiliko mengine ya ngozi yanaweza kujumuisha rangi ya manjano na ongezeko la jasho.
  12. Katika simesta ya pili, matiti huanza kutoa dang’a - dutu ya rangi ya manjano ambayo huwa nene pindi ujauzito unavyoendelea. Dang’a ina wingi wa protini na antibodi za mama, hivyo inafaa kulishwa mtoto kila wakati.

7.9 Mabadiliko katika matiti

Maswali ya Kujitathmini (MK) ya Kipindi cha 7