Maswali ya Kujitathmini (MK) ya Kipindi cha 7

Kwa vile umekamilisha Kipindi hiki, jibu maswali haya ili kutathmini jinsi ulivyofanikiwa katika Malengo ya Mafunzo ya Kipindi hiki. Andika majibu yako katika shajara yako ya masomo na uyajadili na mkufunzi wako katika Mkutano Saidizi wa Somo unaofuata. Unaweza kudhibitisha majibu yako ukilinganisha na vidokezo ulivyoandika katika Maswali ya Kujitathmini yaliyo mwishoni mwa Moduli hii.

Swali la Kujitathmini la 7.1 (hutathmini Malengo ya Mafunzo ya 7.2)

Maumivu ya mgongo husababishwa na nini wakati wa ujauzito?

Answer

Maumivu ya mgongo hutokea mara nyingi katika wanawake wajawazito kwa sababu hali ya mwili wao hubadilika ili kutoa nafasi ya uterasi inayokua. Mgongo hujipinda ndani huku fumbatio likijipinda nje, hivyo kuusukuma mgongo, jambo linaloweza kusababisha maumivu.

Mwisho wa jibu

Swali la Kujitathmini la 7.2 (hutathmini Malengo ya Mafunzo ya 7.3)

Mwanamke mjazito aliongeza kilo 2 za uzito katika wiki 20 za kwanza za ujauzito, kisha kilo 0.5 kila wiki kwa wiki 10 zilizofuata, kisha kilo 0.1 katika wiki 10 za mwisho. Idadi ya jumla ya uzito alioongeza katika mwisho wa muhula wa ujauzito ni gani? Ongezeko hili linadokeza jambo gani linaloendelea?

Answer

Ongezeko la uzito wa mwanamke huyu lilikuwa kawaida katika wiki za kwanza 30 za ujauzito: yeye aliongeza kilo 2 katika wiki 20 za kwanza na kilo 0.5 kila wiki katika wiki 10 zilizofuata. Hata hivyo, mwanamke huyu anatarajiwa kuongeza kilo 0.5 kila wiki kutoka wiki 30 - 40, lakini ongezeko lake la uzito lilipungua hadi kilo 0.1 kwa kila wiki katika kipindi hiki. Haiwezekani kubaini iwapo ongezeko hili mwishoni mwa ujauzito ni dalili ya kuonyesha kuwa fetasi haikui vyema, lakini inafaa kuchunguzwa katika kituo cha afya. Baadhi ya wanawake huwa na mimba ya kawaida bila kuongeza uzito mwingi, lakini kwa wengine hii ni dalili ya kizuizi cha kukua kwa fetasi ndani ya uterasi.

Mwisho wa jibu

Swali la Kujitathmini la 7.3 (hutathmini Malengo ya Mafunzo ya 7.4)

Je, ni kwa nini ni muhimu kwa wanawake wajawazito kula vyakula vilivyo na ayoni kwa wingi au kutumia tembe za ayoni?

Answer

Wanawake wajawazito kwa kawaida hupata anemia ndogo ya kifisiolojia kwa sababu kiasi chao cha damu huongezeka kwa kasi kuzidi ongezeko la idadi ya seli nyekundu za damu. Ayoni huhitajika kwa utoleshaji wa hemoglobini, ambayo ni dutu inayobeba oksijeni katika seli nyekundu za damu. Iwapo mwanamke hana ayoni ya kutosha katika mwili wake, yeye hawezi kutolesha seli nyekundu za kutosha, hivyo anemia yake inaweza kuwa mbaya zaidi. Kula chakula kilicho na ayoni kwa wingi au kumeza tembe zilizo na ayoni ni hatua zinazomsaidia kutolesha seli nyekundu za kutosha kusafirisha oksijeni anayohitaji yeye na fetasi inayokua.

Mwisho wa jibu

Swali la Kujitathmini la 7.4 (hutathmini Malengo ya Mafunzo ya 7.4)

Ni kinachoweza kumfanyikia mwanamke mjamzito iwapo analala chali. Eleza jibu lako

Answer

Mwanamke mjamzito anapolala chali, uzito wa uterasi na vyote vilivyomo hufinya mishipa mikuu ya damu (vena kava) inayotoka upande wa chini wa mwili wake kuelekea moyoni. Jambo hili kwa upande mwingine hupelekea kiwango kidogo zaidi cha damu kupigwa kutoka katika moyo wake hadi sehemu zote za mwili, hivyo shinikizo lake la damu hushuka ghafla. Mwanamke huyu anaweza kupatwa na kizunguzungu au kupoteza fahamu kwa sababu hana oksijeni ya kutosha inayofikia ubongo wake.

Mwisho wa jibu

Swali la Kujitathmini la 7.5 (hutathmini Malengo ya Mafunzo ya 7.5)

Ni habari gani inayoweza kukusaidia kufanya uamizi kuhusu haja ya ushauri wa kiafya wakati mwanamke mjamzito amekumbwa na matatizo ya kupumua?

Answer

Matatizo ya kupumua hutokea mara nyingi katika ujauzito kwa sababu uterasi hukua na kuyasukuma mapafu ya mama, hivyo anakuwa na nafasi ndogo zaidi ya kupumulia. Lakini iwapo mwanamke huyu ni mnyonge, mchovu, na mwenye tatizo la kupumua wakati wote, unafaa kumpa rufaa ili kutafuta ushauri wa kiafya. Mwanamke huyu anaweza kuwa na anemia ama kukumbwa na matatizo ya moyo, au pengine lishe lake ni duni.

Mwisho wa jibu

Swali la Kujitathmini la 7.6 (hutathmini Malengo ya Mafunzo ya 7.1, 7.2, 7.4 na 7.5)

Ni elezo lipi ambalo si kweli?? Katika kila kauli, eleza lisilo la kweli.

  • A.Mwanamke mjamzito huhimizwa kulala bapa baada ya kula kwa sababu hatua hii husaidia katika umeng’enyaji.
  • B.Kukojoa mara kwa mara katika vipindi vya mwishoni mwa ujauzito ni jambo la kawaida kwa sababu uterasi husukuma kibofu.
  • C.Kipimo cha mapigo ya moyo, kiasi cha mshtuko na utoleshaji wa moyo zote huongezeka wakati wa ujauzito.
  • D.Edema katika ujauzito huwa mbaya zaidi wakati wa usiku.
  • E.Rangi inaweza kutokea usoni, ama kama msitari mweusi kwenye fumbatio katika baadhi ya wanawake.
  • F.Watoto wazawa hawafai kulishwa kwa dang’a.
  • G.Projesteroni husababisha uterasi kuongezeka kwa ukubwa ili kuipa nafasi fetasi inayokua.

Answer

A si kweli. Mwanamke mjamzito hahimizwi kulala bapa baada ya kula na hali hii haisaidii katika umeng’enyaji. Vitu vilivyomo tumboni mwa mwanamke mjazito husukumwa kuelekea juu hadi kwenye umio katika kifua anapojilaza, huku asidi inayomeng’enya chakula chake ikisababishwa mwasho unaojulikana kama ‘kiungulia’.

B ni kweli. Kukojoa mara kwa mara katika vipindi vya mwishoni mwa ujauzito ni jambo la kawaida kwa sababu uterasi husukuma kibofu hivyo hakiwezi kuhifadhi kiasi kikubwa cha mkojo.

C ni kweli. Kipimo cha mapigo ya moyo, kiasi cha mshtuko na utoleshaji wa moyo zote huongezeka wakati wa ujauzito. Hii ni kwa sababu mwili wa mwanamke, ambao sasa ni mkubwa zaidi, uterasi na fetasi vyote huhitaji kiasi kukibwa zaidi cha damu ili kuvipa virutubishi na oksijeni.

D si kweli. Edema katika ujauzito kwa kawaida hupungua wakati wa usiku. Viowevu vinavyokusanyika miguuni mwa mwanamke wakati wa mchana hufyonzwa hadi ndani ya mkondo wa damu wakati miguu yake imeinuliwa kitandani wakati wa usiku.

E ni kweli. Rangi inaweza kutokea usoni, ama kama msitari mweusi kwenye fumbatio katika baadhi ya wanawake.

F si kweli. Watoto wazawa wanafaa kulishwa kwa dang’a kila mara. Dang’a ina kiasi cha juu sana cha protini na huwa na antibodi ambazo husaidia kumkinga mtoto kutokana na maambukizi.

G ni kweli. Projesteroni husababisha uterasi kuongezeka kwa ukubwa ili kuipa nafasi fetasi inayokua.

Mwisho wa jibu

Muhtasari wa Kipindi cha 7