Malengo ya Somo la Kipindi cha 7

Baada ya kuhitimisha somo hili, unapaswa kuwa na uwezo wa:

7.1 Kufasili na kutumia kwa usahihi maneno yote muhimu yaliyoandikwa kwa herufi nzito.(Swali la Kujitathmini 7.6 )

7.2 Kueleza mabadiliko ya kifiziolojia ya mfumo wa uzazi wa mwanamke wakati wa ujauzito na athari za mabadiliko haya kwa mwanamke huyu mjamzito. (Maswali ya Kujitathmini 7.1 na 7.6)

7.3 Kueleza mabadiliko wastani ya uzito wa mwili wa mwanamke mjamzito. (Swali la Kujitathmini 7.2)

7.4 Kujadili kuhusu mabadiliko katika mfumo wa moyo na mishipa wakati wa ujauzito, na athari ya shinikizo la damu, utendakazi wa moyo, kiasi cha damu na ukolezi wa seli nyekundu za damu. (Maswali ya Kujitathmini 7.3, 7.4 na 7.6)

7.5 Kubaini mabadiliko ya kawaida na yasio ya kawaida katika mifumo ya pumzi, umeng’enyaji, na mkojo; na pia ngozi, na matiti, ikiwemo utoleshaji wa kolostramu. (Maswali ya Kujitathmini 7.5 na 7.6)

Kipindi cha 7 Mabadiliko ya Kifiziolojia katika Ujauzito

7.1 Mabadiliko ya kifiziolojia katika mfumo wa uzazi wa mwanamke wakati wa ujauzito