7.1 Mabadiliko ya kifiziolojia katika mfumo wa uzazi wa mwanamke wakati wa ujauzito

7.1.1 Mabadiliko katika estrojeni na projesteroni

Katika Kipindi cha 3, 4 na 5 ulijifunza kuhusu homoni kuu za mfumo wa uzazi wa mwanamke, estrojeni na projesteroni, na utendakazi wa homoni hizi katika kuandaa uterasi kudhibiti ujauzito. Vile vile, estrojeni na projesteroni ni homoni kuu katika kipindi chote cha ujauzito.

Mwanamke hutoa estrojeni nyingi wakati wa ujauzito kuliko wakati wowote maishani akiwa hana mimba. Wakati wa ujauzito, estrojeni huimarisha usafirishaji wa damu ya mama ndani ya uterasi na plasenta.

  • Je, estrojeni ina jukumu gani muhimu katika ukuaji wa fetasi?

  • Kwa kuimarisha usafirishaji wa damu ya mama katika uterasi na plasenta, estrojeni huhakikisha kuwa fetasi imesambaziwa virutubishi na oksijeni ili ikue, na kwamba takamwili la fetasi limetolewa kwenye damu ya mama. (Ulijifunza haya katika Kipindi cha 5.)

    Mwisho wa jibu

Pia kiwango cha projesteroni katika mwanamke mjamzito huwa cha juu sana. Miongoni mwa athari zingine, viwango vya juu vya projesteroni husababisha ukubwa wa baadhi ya viungo vya ndani ya mwili kuongezeka, ikiwa ni pamoja na uterasi, ili iweze kubeba mtoto aliyehitimu muhula wote wa ujauzito. Kiwango hiki pia kina athari zingine kwa mishipa ya damu na jointi, ambazo tutajadili baadaye katika Kipindi hiki.

Malengo ya Somo la Kipindi cha 7

7.1.2 Mabadiliko kwenye uterasi, seviksi na uke