7.1.2 Mabadiliko kwenye uterasi, seviksi na uke

Uterasi

Baada ya utungisho, uterasi hutoa mandhari yenye lishe na kinga ambapo fetasi itaweza kukua na kustawi. Uterasi huongezeka kutoka ukubwa sawa na wa pea ndogo wakati mwanamke hana mimba hadi iweze kubeba mtoto aliyehitimu muhula wote wa ujauzito katika wiki 40 za kipindi cha ujauzito. Tishu ambazo hutumika kuunda uterasi huendelea kukua kwa wiki 20 za kwanza na kuongezeka kwa uzito kutoka takriban gramu 50 - 1,000. Baada ya kipindi hiki, uterasi huwa haiongezeki kwa uzito, lakini itajivuta ili kumpa nafasi mtoto anayekua, plasenta na viowevu vya amniotiki. Ujauzito unapohitimisha mwisho wa muhula wake, uterasi itakuwa imeongezeka kwa ukubwa kwa takriban mara tano kuliko ukubwa wake wa kawaida:

  • Kwa urefu (juu hadi chini) kutoka sentimita 7.5 hadi 30.
  • Kwa upana (upande hadi upande) kutoka sentimita 5 hadi 23
  • Kwa urefu (mbele hadi nyuma) kutoka sentimita 2.5 hadi 20.
  • Ni nini husababisha mabadiliko haya?

  • Homoni ya projesteroni hasa husababisha mabadiliko haya.

    Mwisho wa jibu

Katika wiki ya 12 ya ujauzito (karibu mwisho wa trimesta ya kwanza ya ujauzito, yaani kipindi cha miezi mitatu) fandasi (pembeni mwa juu ya mwili wa uterasi) inaweza kupapasika (kuhisika) kupitia fumbatio, juu ya mfupa wa kinena (simfisisi ya kinena). Kwa kawaida, ukubwa wa uterasi hufikia kilele chake baada ya takriban wiki 36 za ujauzito (tazama Mchoro 7.1).

Mchoro 7.1 Urefu wa uterasi katika wiki mbalimbali za ujauzito.
  • Je, ni baada ya wiki ngapi za ujauzito ambapo fandasi ya uterasi inaweza kupapasika katika urefu wa kitovu (kitufe cha fumbatio) cha mwanamke, kulingana na Mchoro 7.1?

  • Kwa takriban wiki 20.

    Mwisho wa jibu

Kichwa cha fetasi kinapojitandaza kwenye pelvisi kwa maandalizi ya kuzaliwa, uterasi inaweza kushuka kidogo. Makinika kuhusu hali ya fetasi katika wiki 40, ambapo imeonyeshwa kwa alama ya mstari wa vitone kwenye Mchoro 7.1. Kushuka huku hujulikana kama 'kuwepesuka'. Hali hii huonekana wazi katika mama primigravida (mjamzito kwa mara ya kwanza) kuliko maltigravida (mwanamke aliyewahi kuwa mjamzito awali, bila kuzingatia Malengo ya ujauzito huu).

Seviksi

Seviksi hubakia na urefu wa sentimita 2.5 katika kipindi chote cha ujauzito. Katika kipindi cha mwishoni mwa ujauzito, seviksi hunyooka kufuatia mikazo isiyo chungu ya pembezo zake inayoongezeka.

Uke

Inapoakaribia mwisho wa ujauzito, uke pia huendelea kunyumbulika. Mabadiliko haya huwezesha uke kutanuka katika awamu ya pili ya leba, huku mtoto akishukia katika njia ya uzazi. (Utajifunza kuhusu haya yote katika Moduli inayofuata ya Leba na Utunzaji wakati wa Kuzaa.)

7.1 Mabadiliko ya kifiziolojia katika mfumo wa uzazi wa mwanamke wakati wa ujauzito

7.2 Mabadiliko ya mkao na viungo vinavyohusiana na ujauzito