7.2 Mabadiliko ya mkao na viungo vinavyohusiana na ujauzito

Mtoto anapoendelea kukua, mkao wa kijumla wa mama mjamzito hubadilika. Fumbatio lake hubadilika kutoka hali bapa au ya kubonyea (kama bakuli) hadi kubinuka sana (kutokeza nje). Hali hii husababisha kuongezeka kwa mpindiko wa mgongo wake. Uzito wa fetasi, kuongezeka kwa uterasi, plasenta na kiowevu cha amniotiki (kifuko cha maji kinachozingira mtoto), pamoja na ongezeko la mpindiko wa mgongo wake, yote husukuma mifupa na misuli ya mwanamke. Kufuatia hali hii, wanawake wengi wajawazito hukumbwa na maumivu ya mgongo. Kusimama kwa muda mrefu mahali pamoja au kuinamia mbele kunaweza kusababisha maumivu ya mgongo, na vivyo hivyo pia kujishugulisha katika kazi ngumu. Aina nyingi za maumivu ya mgongo wakati wa ujauzito ni kawaida, ingawa yanaweza kuwa viashirio hatari ya maambukizi ya figo. (Utajifunza jinsi ya kutambua maambukizi ya figo katika Kipindi cha 18.)

Vile vile, projesteroni husababisha ulegevu wa ligamenti na viungo katika mwili wote. Wanawake wajawazito wanaweza kuwa katika hatari ya kuteguka na kusukumika kwa sababu ligamenti zao ni legevu, na kwa kuwa mkao wake umebadilika.

7.1.2 Mabadiliko kwenye uterasi, seviksi na uke

7.3 Mabadiliko ya uzani katika ujauzito