7.3 Mabadiliko ya uzani katika ujauzito

Kuendelea kuongezeka kwa uzani wakati wa ujauzito hukisiwa kuwa mojawapo ya viashirio kuwa mwili wa mama unaanza kukubali mabadiliko na kukua kwa fetasi. Hata hivyo, upimaji wa uzani wa mama mara kwa mara wakati wa ujauzito kwa sasa umeonekana kutokuwa muhimu, kwa sababu haulingani vyema na Malengo ya ujauzito. Kwa mfano, mwanamke anaweza kushusha uzani wake kwa kiasi katika kipindi cha mwanzo wa ujauzito ikiwa alipata kichefuchefu na kutapika sana (mara nyingi huitwa‘ugonjwa wa asubuhi’). Utajifunza mengi kuhusu haya na matatizo mengine madogo ya ujauzito katika Kipindi cha 12, baadaye katika Moduli hii. Ongezeko la uzani linalotarajiwa katika mwanamke mwenye afya nzuri, aliye na mimba ya hali ya wastani na aliyebeba mtoto mmoja ni kama ifuatayo:

  • Takriban kilogramu 2.0 kwa jumla katika wiki 20 za kwanza.
  • Kisha takriban kilogramu 0.5 kila wiki hadi kipindi cha ujauzito kutimia wiki 40.
  • Jumla ya kilogramu 9-12 wakati wa ujauzito.

Mwanamke aliye na ujauzito wa zaidi ya mtoto mmoja atakuwa na ongezeko kubwa zaidi la uzani akilinganishwa na aliye na fetasi moja. Mwanamke huyu pia atahitaji chakula chenye kalori nyingi zaidi. (Utajifunza mengi kuhusu chakula na lishe bora na ujauzito katika Kipindi cha 14 katika Moduli hii.)

Ukosefu wa ongezeko bayana la uzito hautakuwa jambo la kusababisha wasiwasi kwa baadhi ya wanawake, lakini linaweza kuwa kiashirio kuwa fetasi haikui vyema. Daktari na wakunga wanaweza kuita jambo hili udumavu wa ukuaji wa mtoto katika uterasi.

7.2 Mabadiliko ya mkao na viungo vinavyohusiana na ujauzito

7.4 Mabadiliko katika mfumo wa moyo na mishipa