7.4 Mabadiliko katika mfumo wa moyo na mishipa

Mfumo wa moyo na mishipa unajumuisha moyo, mishipa ya damu (vena na ateri), na damu inayozunguka mwilini. Huu ni mfumo wa usafirishaji mwilini unaofikisha oksijeni na virutubishi kutoka katika mfumo wa tumbo na utumbo mdogo hadi katika seli, tishu na viungo vya mwili ili kuwezesha kuzalisha nguvu zinazohitajika katika utendakazi wa mwili. Mfumo huu pia hurudisha dioksidi ya kaboni, ambayo ni aina ya takamwili inayofuatia pumzi, hadi kwenye pafu, ili kutolewa kwa njia ya kupumua. Taratibu za kikemikali zinazoendelea mwilini hutoa taka nyingi ambazo husafirishwa kwa damu hadi kwenye figo na ini ambapo huondolewa. Kazi zingine za mfumo wa moyo na mishipa ni pamoja na kudhibiti joto mwilini, kusafirisha na kufikisha homoni na chembechembe zingine zinazodhibiti utendakazi wa mwili. Kuna mabadiliko makubwa katika mfumo huu tata wakati wa ujauzito.

7.3 Mabadiliko ya uzani katika ujauzito