7.4.1 Moyo

Moyo unaweza kuongezeka kwa ukubwa wakati wa ujauzito kutokana na kuongezeka kwa kazi yake.

  • Unafikiri ni kwa nini kazi ya moyo ni sharti iongezeke?

  • Hii ni kwa sababu moyo unapaswa kusambaza damu kupitia plasenta, fetasi na uterasi na fumbatio la mwanamke mjamzito.

    Mwisho wa jibu

Kiwango cha damu kinachopigwa kutoka katika moyo kila dakika huitwa uzalishaji wa moyo. Jedwali 7.1 linaonyesha jinsi kazi ya moyo inavyoongezeka katika ujauzito.

Jedwali 7.1 Mabadiliko ya uzalishaji wa moyo katika ujauzito
Hali ya mwanamkeUzalishaji wa moyo (lita kwa kila dakikia)
Mwanamke asiye mjamzito, aliye katika hali tulivu2.5
Mwisho wa awamu ya kwanza ya ujauzito5
Mwisho wa awamu ya pili ya ujauzito6
Muhula wote wa ujauzito7

Ongezeko la uzalishaji wa moyo husababishwa na mabadiliko mawili katika jinsi moyo unavyotenda kazi:

  • Ongezeko la kima cha mapigo ya moyo katika hali ya kutulia, yaani idadi ya midundo ya moyo kwa kila dakika. Kima cha mapigo ya moyo ni takriban midundo 15 zaidi kwa kila dakika kwa mwanamke mjamzito.
  • Ongezeko la kiasi cha kipigo, yaani, kiasi cha damu kinachopigwa kutoka katika moyo kwa kila mdundo. Kiwango hiki ni takriban mililita 7 zaidi kwa kila mdundo katika mwanamke mjamzito.

Uzalishaji wa moyo hukokotolewa kwa kuzidisha kiwango cha upigaji moyo na kiasi cha kipigo.

Katika awamu ya pili ya ujauzito, mama akiwa ametulia, moyo wake hufanya kazi kwa asilimia 40 zaidi kuliko akiwa hana mimba. Kiwango kikubwa cha ongezeko hili hutokea kufuatia moyo unaotenda kazi kifasaha, ambao hupiga damu zaidi kwa kila mdundo.

7.4 Mabadiliko katika mfumo wa moyo na mishipa

7.4.2 Kiasi cha damu