7.4.4 Mazoezi na mtiririko wa damu wakati wa ujauzito

Ongezeko la uzito katika mwanamke mjamzito huzidisha utendakazi wa mwili kufuatia mazoezi yoyote. Mazoezi taratibu yasiyo makali ni bora kwa mama kwa sababu mazoezi haya huandaa mwili wake kuhimili leba. Mazoezi makali ya ghafla, au kufanya kazi kwa muda mrefu bila kupumzika ni jambo linaloweza kumfanya ahisi kizunguzungu. Hisia hizi hutokea kwa sababu shinikizo la chini la damu na anemia ndogo ya kifiziolojia haiwezi kutosheleza kiwango cha ziada cha oksijeni kinachohitajika mwilini.

Kielelezo 7.2 Mwanamke mjamzito anafaa kujiepusha na mazoezi mazito au mepesi mno.

Mwanamke mjamzito hafai kufanya mazoezi ambapo amelala chali, kwa sababu mishipa mikuu inayorudisha damu moyoni itafinyika. Mazoezi makali yanaweza kupelekea upungufu wa damu inayotiririka kwenye uterasi kwa sababu damu itaelekezwa kwenye misuli, ingawa jambo hili halijaonekana kuwa na athari ya kudumu kwa mtoto. Wanawake wajawazito hawapaswi kufanya mazoezi makali katika msimu wa joto kali, au ikiwa mazoezi hayo yatamfanya asipumue vizuri au kama kuna hatari zozote zinazojulikana kama vile, historia ya utokaji mimba ghafla.

7.4.3 Shinikizo la damu katika ujauzito

7.4.5 Edema wakati wa ujauzito