7.4.5 Edema wakati wa ujauzito

Edema hutamkwa kwa "ii diii mah".

Ikiwa mwanamke mjamzito atakumbwa na edema, kali ikiwemo kufura uso, hii ni dalili ya hatari inayohitaji mama kupelekwa kwa dharura hadi kituo cha afya kilicho karibu.

Ongezeko la uwezo wa mishipa midogo ya damu kupenyeka (yaani mishipa kuruhusu viowevu vingi kuvuja nje hadi katika tishu) na uzito wa ziada wa uterasi, na mvuto wa graviti hudhoofisha kima cha kusambaza damu kurudi moyoni kutoka katika sehemu ya chini ya mwili. Mara nyingi viowevu hukusanyika kwenye tishu ya miguu ya mwanamke mjamzito baada ya kipindi cha kwanza cha ujauzito, badala ya kufyonzwa iingie kwenye mfumo wa mzunguko wa damu. Kufura kunakosababishwa na mkusanyiko wa viowevu hivi huitwa edema.

Edema ni hali ya kawaida kwa wanawake wajawazito, hususan wakisimama kwa muda mrefu. Pia, edema ya mikono inaweza kutokea. Mshauri mama apumzike mara kwa mara na kuhakikisha ameiinua miguu yake akiwa ameketi. Jambo hili litaimarisha uwezo wa damu yake kurudi moyoni na pia kumsaidia kupunguza kufura kwa miguu.

7.4.4 Mazoezi na mtiririko wa damu wakati wa ujauzito

7.5 Mabadiliko ya kipumzi