7.5 Mabadiliko ya kipumzi

Wakati wa ujauzito, kiasi cha hewa inayoingia na kutoka katika mapafu huongezeka kwa karibu asilimia 50 kwa sababu hizi mbili:

  • Kila upumuo una kiasi kikubwa zaidi cha hewa
  • Kima cha kupumua (pumzi kwa dakika) huongezeka kwa kiasi kidogo.

Wakati wa ujauzito, wanawake wengi hutambua kwamba wanakumbwa na matatizo ya kupumua (hawawezi kuvuta ndani pumzi nyingi kama kawaida). Hii ni kwa sababu mtoto anayekua husukuma mapafu ya mama, hivyo ana nafasi ndogo zaidi ya kupumua. Lakini iwapo pia ni mnyonge na mchovu, ama amekosa hewa ya kutosha wakati huu wote, anafaa kuchunguzwa ili kubaini kama ana maradhi, matatizo ya moyo au lishe duni. Pata ushauri wa daktari iwapo unadhani kuwa anaweza kuwa na mojawapo ya hali hizi.

7.4.5 Edema wakati wa ujauzito

7.6 Mabadiliko katika mfumo wa tumbo na utumbo wakati wa ujauzito