7.6 Mabadiliko katika mfumo wa tumbo na utumbo wakati wa ujauzito

Kama unavyoweza kukumbuka kutoka masomo yako ya shule ya upili ya bayolojia, chakula na viowevu huingia katika mfumo wa tumbo na utumbo kupitia mdomo, kisha kupitia umio, tumbo na utumbo, kisha taka ngumu ikatolewa katika kinyeo. Mkanda huu ulio mrefu sana kutoka mdomoni hadi kinyeo mara nyingi hujulikana kama ’utumbo’. Protini, mafuta na kabohidreti katika lishe huvunjwavunjwa (kumeng’enywa) katika utumbo hadi kuwa vipande vidogo sana vinavyoweza kufyonzwa kutoka utumboni hadi katika mishipa ya damu. Hii pia ndiyo njia ambayo dutu zenye rutuba, kama vile vitamini na madini huingia mwilini.

Wakati wa ujauzito, misuli ya pembezo za mfumo wa tumbo na utumbo hulegea kidogo, kisha kima cha kufinyia chakula nje ya tumbo na katika utumbo hupungua kidogo.

  • Je, unaweza kutaja sababu inayofanya upungufu wa mwendo wa chakula katika mfumo wa tumbo na utumbo kuwa na manufaa wakati wa ujauzito?

  • Upungufu huu wa mwendo wa chakula huongeza muda wa umeng’enyaji ili kuwezesha ufyonzaji wa kutosha wa virutubishi katika lishe.

    Mwisho wa jibu

Athari mbaya pia husababishwa na mwendo wa polepole wa kuondoa chakula katika tumbo na utumbo wote.

  • Hebu taja mojawapo ya athari hizi mbaya.

  • Wanawake wengi wajawazito hupatwa na hali ya kufunga choo (ugumu wa kuondoa kinyesi).

    Mwisho wa jibu

Kielelezo 7.3 Ukuaji wa mtoto huziba fumbatio la mama, jambo linaloweza kusababisha matatizo ya umeng’enyaji na kiungulia. Mwanamke huyu pia anaweza kushindwa kupumua vyema kwa sababu mtoto ameyasukuma mapafu.

Wanawake wengi pia huwa na kichefuchefu katika miezi ya kwanza ya ujauzito. Hisia za kuchomeka au maumivu tumboni au katikati ya matiti hujulikana kama ukosefu wa umeng’enyaji (au ’kiungulia’, ingawa moyo kwa kawaida haiathiriwi). Kiungulia hutokea kwa sababu pindi mimba inavyoendelea, mtoto anayekua hujaza fumbatio la mama hivyo kulisukuma juu kuliko kawaida (Kielelezo 7.3). Asidi zilizo katika fumbatio la mama zinazosaidia kumeng’enya chakula husukumwa hadi sehemu ya juu kifuani, ambapo zinasababisha hisia za kuchomeka. Hali hii si hatari na kwa kawaida huisha baada ya kuzaa.

Iwapo mama huyu ana matatizo ya kichefuchefu na umeng’enyaji, mshauri kula chakula kidogo mara nyingi. Mama huyu hafai kulala bapa kwa saa 1 - 2 baada ya kula, kwa sababu jambo hili linaweza kusababisha hali hizi. Katika Kipindi cha 12, utajifunza zaidi kuhusu matatizo madogo ya ujauzito kama hizi, na jinsi ya kumsaidia mwanamke huyu kuzidhibiti.

7.5 Mabadiliko ya kipumzi

7.7 Mabadiliko katika mfumo wa mkojo wakati wa ujauzito