7.7 Mabadiliko katika mfumo wa mkojo wakati wa ujauzito

Mfumo wa mkojohuwa na figo (jozi la viungo katika pande zote mbili za fumbatio karibu na mgongo), mishipa inayounganisha figo hizi na kibofu ambapo mkojo huhifadhiwa, na mshipa unaojulikana kama urethra unaopitisha mkojo nje ya mwili. (Rejelea Kielelezo 3.1 katika Kipindi cha 3 ili kujikumbusha kuhusu nafasi ya kibofu na urethra.) Figo hutoa taka katika damu na kuligeuza kuwa mkojo. Ni sharti figo kufanya kazi ya ziada ili kulichunga taka la mama mwenyewe kutoka katika damu yake, na pia taka ya fetasi, na kisha kuliondoa kupitia mkojo wake. Kwa hivyo, pia kuna ongezeko la kiasi cha mkojo unaotolewa na mama wakati wa ujauzito.

Ni jambo la kawaida kwa mwanamke kukojoa mara nyingi, hasa katika miezi ya kwanza na ya mwisho ya ujauzito. Jambo hili hufanyika kwa sababu fetasi inasukuma kibofu. Mwishoni wa ujauzito, mara nyingi mwanamke huhitaji kuamka usiku ili kukojoa. Hii ni kwa sababu kiowevu kilichokusanyika miguuni na nyayoni wakati wa mchana (edema) hufyonzwa katika damu miguu yake inapoinuliwa kitandani. Figo hufyonza viowevu hivi vya ziada kisha kuvigeuza kuwa mkojo, hivyo kibofu hujazwa haraka zaidi wakati wa usiku.

7.6 Mabadiliko katika mfumo wa tumbo na utumbo wakati wa ujauzito

7.8 Mabadiliko ya ngozi