Malengo ya Somo la Kipindi cha 8

Baada ya kipindi hiki unapswa kuweza:

8.1 Kufafanua na kutumia kwa usahihi maneno yote muhimu yalioandikwa kwa herufi nzito. (Maswali ya Kujitathmini 8.1 na 8.4)

8.2 Kueleza kwa nini ni muhimu kupata imani na uhakika wa mwanamke anayekuja kwako kwa utunzaji katika ujauzito, na utoe mfano wa jinsi unavyoweza kudumisha au kupoteza imani yake. (Swali la Kujitathmini 8.1)

8.3 Kutofautisha kati ya ishara za ujauzito zinazoweza kutokea, zinazoelekea kutokea na zile chanya, na uamue ikiwa mwanamke ana uwezekano au anaelekea kuwa mjamzito kwa msingi wa uchunguzi kifani wa kubuni. (Swali la Kujitathmini 8.2)

8.4 Kuuliza maswali wazi nawanayoelewa ili kukusaidia kupata habari kuhusu dalili za ujauzito zinazoweza kuonekana au visababishi vya hatari vinavyotokea sana na vinavyoweza kuathiri afya ya mwanamke mjamzito au mtoto wake. (Maswali ya Kujitathmini 8.1 na 8.5)

8.5 Kutambua visababishi vikali vya hatari vinavyoweza kupelekea mwanamke huyo kuhitaji kuzalia kwenye kituo cha afya kuliko nyumbani. (Maswali ya Kujitathmini 8.3 na 8.4)

Kipindi cha 8 Kutambua ujauzito na Kujifunza Historia ya Mwanamke Mjamzito

8.1 Kupata imani ya mwanamke katika utunzaji katika Ujauzito