8.2 Kutambua iwapo mwanamke ni mjamzito

Viashiria vya ujauzito vimeainishwa kijumla katika makundi matatu:

  • Dalili zinazoweza kuashiria ujauzito: mabadiliko katika mwili wake ambayo mwanamke anaweza kutambua mwenyewe na akuambie kuhusu yanayoweza kumaanisha kuwa ni mjamzito lakini yanaweza pia kusababishwa na jambo jingine. Ripoti ya dhahania ya mwanamke huyo ndiyo uliyo nayo tu ya kukusaidia katika utambuzi wako. Hata hivyo, katika kituo cha afya, dalili zinazoweza kutokea huwa ndio ushahidi uliopo katika miezi ya kwanza mitatu hadi sita.
  • Ishara na dalilizinazoelekeakuashiria ujauzito: baadhi ya viashiria hivi huripotiwa na mwanamke huyo lakini pia unaweza kujionea mwenyewe. Pia kuna kipimo cha ujauzito unachoweza kufanya au kinachoweza kufanywa katika kituo cha afya cha kiwango kinachofuata.
  • Dalili chanya za ujauzito: hizi ni ithibati kamili ya ujauzito kwa msingi wa utambuzi halisi.

8.1 Kupata imani ya mwanamke katika utunzaji katika Ujauzito

8.2.1 Dalili zinazoweza kuashiria ujauzito