8.3.1 Je, ana miaka mingapi?

Ujauzito unaweza kusababisha matatizo kwa wanawake wa umri wowote. Lakini wanawake wa umri mdogo sana na wenye umri mkubwa sana huwa na matatizo zaidi.

Wasichana wanaopata ujauzito kabla ya umri wa miaka 17 wanaweza kuwa hawajamaliza kukua. Huenda pelvisi ya msichana haijakua vya kutosha kuweza kuzaa kikawaida. Wasichana wana uwezekano mkubwa wa kuwa na matatizo pia - kama priklampsia (tazama Jedwali 8.2), leba ya muda mrefu na watoto wanaozaliwa mapema sana. Wasichana wanaopata ujauzito wakiwa wachanga sana wanaweza kuwa mama wazuri sana na watunzaji, hata hivyo wengi wao watahitaji ushauri na usaidizi zaidi.

Inaweza kuwa salama kwa wanawake walio na umri mkubwa sana na wenye umri mdogo sana kuzalia katika kituo cha afya kilicho na vifaa, kuliko nyumbani.

Wanawake wakongwe wanaweza pia kuwa na matatizo zaidi katika ujauzito na kuzaa.

Kisanduku 8.2 Priklampsia na eklampsia

Priklampsia ni hali hatari inayojulikana kwa shinikizo la juu la damu (hipatensheni), kufura mikono, miguu na hata uso, na kiwango cha haja cha protini katika mkojo (protinuria). Kwa kawaida hutokea katika miezi mitatu ya mwisho ya ujauzito. Wanawake walio na ugojwa huu huhisi kuugua sana na mara nyingi wao huripoti maumivu makali ya kichwa, kichefuchefu, na kutapika.

Ukishuku kuwa mwanamke mjamzito ana priklampsia, unapaswa kumpa rufaa aende katika kituo cha afya kilicho karibu mara moja.

Priklampsia isipotibiwa inaweza kuendelea na kuwa eklampsia ambapo dalili hizo zote huwa mbaya zaidi na mwanamke huyo kupata kuchanganyikiwa kiakili, matatizo katika kuona na matukutiko. Eklampsia ni hatari kwa maisha ya mwanamke na mtoto wake ambaye bado hajazaliwa.

Eklampsia, priklampsia, na aina zingine za magonjwa yanayosababishwa na shinikizo la juu la damu hujulikana kama magonjwa ya hipatensheni, yamejadiliwa kwa kina katika Kipindi cha 19.

8.3 Kutambua mambo yanayoweza kusababisha hatari katika ujauzito

8.3.2 Je, amezaa watoto wangapi awali?