8.3.3 Je, ujauzito wake umewahi kuharibika?

Wanawake wengine hupata ujauzito unaoharibika mmoja baada ya mwingine, na huenda usijue kisababishi. Mpe rufaa aende katika kituo cha afya kilicho karibu ili kujua kisababishi na pia kumsaidia kubeba ujauzito huu hadi mwisho.

Kuharibika kwa ujauzito (ujauzito kutoka wenyewe) ni ambapo ujauzito unatoka kabla ya mwanamke kufikisha majuma 28, mtoto akiwa angali mdogo sana kuweza kuishi nje ya mama bila huduma maalum ya dawa za uangalizi makini wa wagonjwa hospitalini. Uharibikaji wa ujauzito hutokea sana na mara nyingi hutendeka hata kabla ya mwanamke kujua kuwa ana ujauzito.

Huwa vigumu kujua sababu ya kuharibika kwa ujauzito. Lakini visababishi vingine vinaweza kukingwa. Malaria, maambukizi ya zinaa, jeraha, vurugu na dhiki vyote vinaweza kusababisha kuharibika kwa ujauzito.Wakati mwingine, kuharibika kwa ujauzito hutokea mwanamke anapotangamana na sumu au kemikali zenye sumu. Kwa mfano, wanawake wanaofanya kazi kwenye mashamba hupumua au kushika dawa za kuua wadudu mara kwa mara. Hivyo basi kupelekea uharibikaji mwingi wa ujauzito kuliko wanawake wasiotangamana na kemikali hizo. Baadhi ya uharibikaji wa ujauzito unaweza kuzuiwa kwa kuwatibu wanawake walio na magonjwa au maambukizi, au kuwasaidia kuepuka kemikali au dhuluma.

8.3.2 Je, amezaa watoto wangapi awali?

8.3.4 Je, amewahi kutoa mimba?