8.3.4 Je, amewahi kutoa mimba?

Mwanamke aliyekuwa mgonjwa, aliyepata jeraha au aliyetokwa na damu nyingi baada ya aina yoyote ya uavyaji wa ujauzito anaweza kuwa na kovu kwenye uterasi yake zinazoweza kusababisha matatizo katika ujauzito huu au kuzaa. Huenda ni salama kwake kuzalia hospitalini.

Ikiwa mtu yeyote au mwanamke mwenyewe atafanya lolote kwenye mwili wake ili kuuharibu ujauzito, itaitwa utoaji wa mimba. Ambapo uavyaji wa mimba ni halali na unapatikana, mwanamke anaweza kuavya mimba salama na kutohatarisha ujauzito utakaofuata.

Mahali ambapo utoaji wa mimba si halali, mwanamke anayejaribu kuharibu ujauzito anaweza kujidhuru au kumwendea mtu asiyeweza kuavya mimba kwa usalama (Jedwali 8.4). Uavyaji mimba usio salama unaweza kusababisha kutokwa na damu nyingi, maambukizi mabaya, utasa, au hata kifo. Kipindi cha 20 kitakufundisha jinsi ya kumhudumia mwanamke baada ya utoaji mimba usio salama.

Picha 8.4 Maambukizi ni hatari sana hasa kutokana na utoaji mimba usio salama kwa sababu vidole au vyombo vichafu vinaweza kuingizwa kwenye mwili wa mwanamke huyo.

8.3.3 Je, ujauzito wake umewahi kuharibika?

8.3.5 Je, amewahi kupata matatizo yoyote ya kuzaa au ujauzito wa awali?