8.3.6 Je, anayo matatizo mengine yoyote ya kiafya?

Wanawake wengi ni wenye afya na wanaweza kuzaa bila hatari yoyote kuwapata pamoja na watoto wao. Hata hivyo, ni sehemu muhimu ya jukumu lako kama mtaalam wa afya kuwajua wanawake walio katika hatari kubwa kwa sababu ya matatizo waliyo nayo au waliyokuwa nayo. Ikiwa mwanamke mjamzito ni mgonjwa anayekumbwa na mojawapo ya matatizo haya, wakati huu au uliopita, anafaa kupata usaidizi wa kiafya ili kupangia mahitaji yake katika ujauzito na kuamua ikiwa atazalia hospitalini:

  • Kisukari melitasi
  • VVU/ UKIMWI
  • Maambukizi ya kibofu au figo
  • Malaria
  • Kiwango juu cha joto zaidi ya sentigredi 37.5 (100.4 F) kwa zaidi ya siku mbili, au kiwango juu cha joto cha mara kwa mara
  • Shinikizo la juu la damu
  • Priklampsia na eklampsia
  • Ugonjwa wa ini (hepatitisi hasa hepatitisi B)
  • Matatizo ya moyo
  • Kifua kikuu ambacho hakijatibiwa
  • Ulemavu kwenye nyonga au chini ya mgongo.

8.3.5 Je, amewahi kupata matatizo yoyote ya kuzaa au ujauzito wa awali?

8.3.7 Maswali yako mwenyewe