9.8 Kuchunguza ugonjwa wa kisukari

Wakati mama ana ugonjwa wa kisukari, mwili wake hauwezi kutumia sukari yote kwa damu, hivyo inakaa juu sana na baadhi yake inaweza kuonekana kwa mkojo wake.

Ishara na dalili za hatari

Kama mama ana baadhi ya dalili za hatari zifuatazo, anaweza kuwa na ugonjwa wa kisukari. Kina mama wanaougua ugonjwa wa kisukari kwa kawaida hawana ishara hizi zote. Lakini vile mama ana dalili zaidi, ndivyo kuna uwezekano mkubwa kwamba ana ugonjwa wa kisukari.

Mchoro 9.13 Kukojoa mara kwa mara kunaweza kuwa onyo la dalili ya ugonjwa wa kisukari.
  • Alikuwa na ugonjwa wa kisukari katika ujauzito wa awali.
  • Mmoja wa watoto waliozaliwa alikuwa mkubwa sana (zaidi ya kilo 4); hii ni kwa sababu sukari nyingi katika damu ya mama humfanya mtoto kuongeza uzito kupita kiasi.
  • Mmoja wa watoto wake alikuwa mgonjwa sana au alikufa wakati wa kuzaliwa bila kujua sababu.
  • Yeye ni mnene.
  • Yeye hupatwa na kiu kila wakati.
  • Yeye huwashwa mara kwa mara na ana harufu mbaya inayotoka kwa uke wake.
  • Majeraha yake hupona polepole.
  • Yeye hukojoa mara kwa mara zaidi kuliko wajawazito wengine (Mchoro 9.13).
  • Uterasi yake ni kubwa kuliko ya kawaida kutokana na ile miezi amekuwa mjamzito.

9.7.1 Jinsi ya kupima shinikizo la damu

9.8.1 Vipimo vya mkojo kwa ugonjwa wa kisukari