9.9 Kuchunguza maambukizi ukeni

Mchozo wa kawaida ukeni haunuki, iko kiasi kidogo, na haiweki doa wala kulowesha chupi.

Dalili za hatari

Ikiwa mama ana maambukizi ukeni, ishara ni:

  • Mchozo mweupe unaoonekana kama maziwa ya mgando
  • Mchozo ulio na harufu mbaya
  • Kuwasha kwa sehemu ya nje ya uzazi (angalia nyuma katika Mchoro 3.2 kwa Kipindi cha 3 ili kujikumbusha kuhusu anatomi ya sehemu ya jenitalia ya wanawake)
  • Vulva inaweza kuwa na uvimbe
  • Kunaweza kuwa na uchungu wakati wa kukojoa
  • Mama anaweza kuripoti ana maumivu wakati wa ngono

Ikiwa mama anamchozo ambayo sio ya kawaida, au anaripoti dalili zozote zingine zilizotajwa hapo awali, mpe rufaa kwenye kituo cha afya kilicho karibu haraka iwezekanavyo.

9.8.2 Jinsi ya kumsaidia mama aliye na ugonjwa wa kisukari

9.10 Hitimisho