9.10 Hitimisho

Katika Kipindi hiki, umejifunza jinsi ya kufanya utathmini wa kawaida kwa mama mjamzito anapotembelea kliniki ya wajawazito, na kutambua dalili za afya au dalili na ishara hatari na hatua ambazo unaweza kuchukua. Umejifunza jinsi ya kutathmini kina mama kwa hali duni ya lishe, weupe, ugumu wa kupumua, shinikizo la juu la damu, joto jingi mwilini, ugonjwa wa kisukari, na maambukizi ukeni. Umejifunza jinsi ya kupima joto, mpigo na shinikizo la damu, na kupima sukari kwa mkojo. Katika Kipindi kijacho, utajifunza jinsi ya kufanya uchunguzi wa fumbatio ya mama mjamzito kupima ukubwa wa uterasi yake. Hii inakusaidia kutambua kama fetasi inakuwa kwa njia ya kawaida wakati wa ujauzito.

9.9 Kuchunguza maambukizi ukeni

Muhtasari wa Kipindi cha 9