Maswali za Kujitathmini ya Kipindi cha 9
Kwa vile umekamilisha Kipindi hiki, unaweza kutathmini jinsi ulivyopata mafanikio yake ya Matokeo ya Kujifunza kwa kujibu maswali haya. Andika majibu yako kwa Shajara lako la Somo na uyajadili na Mkufunzi wako katika Mkutano ujao wa Somo Saidizi. Unaweza kulinganisha majibu yako na Maelezo kwa Maswali ya Kujitathmini mwishoni mwa moduli hii.
Swali la Kujitathmini 9.1 (linatathmini Malengao ya Somo la 9.1)
Linganisha kila utambuzi na ishara au dalili hatari inayohusishwa.
Using the following two lists, match each numbered item with the correct letter.
Weupe
Uvimbe shingoni
Joto jingi mwilini
Uterasi kubwa kuliko iliyotarajiwa kwa hatua ya mimba
Shinikizo la juu la damu
a.Ugonjwa wa kisukari
b.Tezi
c.Prekilampsia
d.Malaria
e.Anemia
- 1 = e
- 2 = b
- 3 = d
- 4 = a
- 5 = c
Swali la Kujitahmini 9.2 (linatathmini Malengo ya Somo 9.2 na 9.3)
Je, taarifa zipi zifuatazo si kweli? Katika kila hali, sema kwa ni nini sio sahihi.
- A.Tezi kwa wajawazito husababishwa na upungufu wa madini ya ioni.
- B.Ugonjwa wa kisukari kwa wajawazito mara nyingi husababisha mtoto kuzaliwa akiwa mkubwa.
- C.Upungufu wa pumzi inaweza kusababishwa na anemia, matatizo ya moyo, maambukizi ya mapafu, au kuganda kwa damu.
- D.Shinikizo la damu ya mmHg 90/50 ni dalili ya afya bora.
- E.Kiwango cha mpigo kwa mshipa wa midundo 80 kwa dakika au chini inawezea kuwa ishara hatari ya anemia.
- F.Shinikizo la damu na kiwango cha mdundo kwa mishipa zinapaswa kupimwa wakati mama ameketi akiwa ametulia.
Answer
A si kweli. Tezi husababishwa na upungufu wa madini ya iodini, na si ya ioni.
B ni kweli. Kisukari kwa mjamzito matokeo yake mara nyingi huwa ni mtoto mkubwa kwa sababu mama ana sukari nyingi mwilini, ambayo inamfanya mtoto awe mnene
C ni kweli. Ugumu wa kupumua unaweza sababishwa na anemia, matatizo ya moyo, maambukizi kwa mapafu, au donge la damu.
D si kweli. Shinikizo la damu la mmHg 90/50 liko chini sana, na ni ishara ya hali ya kutokwa na damu nyingi au mshtuko. Katika hali kama hiyo mama lazima apewe rufaa kwenye kituo cha afya mara moja.
E si kweli. Mdundo kwa mshipa wa kawaida wakati mama anapopumzika huwa mipigo 60-80 kwa dakika. Mipigo ya kasi (midundo 100 kwa dakika au zaidi) inaweza kuwa ishara ya anemia.
F ni kweli. Shinikizo la damu na kiwango cha Mpigo zinapaswa kupimwa wakati mama ameketi akiwa ametulia.
Mwisho wa jibu
Swali la Kujitahmini 9.3 (linatathmini Malengo ya Somo la 9.2 na 9.3)
Wakati wa kipindi kabla ya kuzaliwa unapoenda kumwona Zufan, nakili vipimo vifuatafuatavyo:
- Joto: Nyuzi 37.2
- Kiwango cha mipigo kwa mshipa: midundo 96 kwa dakika
- Shinikizo la damu: mmHg 142/100
Je, unapaswa kumpa Zufan rufaa kwa kituo cha afya? Eleza ni kwa nini unapaswa au haupaswi kumpa Zufan rufaa kwa kituo cha afya.
Answer
Unapaswa kumpa rufaa Zufan mara moja. Ingawa joto lake liko karibu na ya kawaida na hatoi waziwazi, mipigo yake kwa mshipa wako kwa kiwango cha kasi kuliko ya kawaida, na shinikizo lake la damu liko juu sana – nambari ya juu na ya chini zote zimezidi kiwango cha onyo ya mmHg 140/90.
Mwisho wa jibu
Muhtasari wa Kipindi cha 9