9.1 Kuangalia dalili za lishe duni au ukosefu wa madini ya iodini

Unapoanza huduma ya ujauzito, mmoja kati ya mambo unayopaswa kuuliza kwanza mjamzito ni kama ana dalili zozote zinazoashiria lishe duni au ukosefu wa madini ya iodini kwa mlo wake. Hii ni muhimu sana, kwa sababu lishe duni kwa mama huhusishwa na matokeo duni ya mimba kama vile mtoto mdogo, na anaweza kuwa mfupi. Maswali unayomuuliza lazima ya lenge kugundua iwapo ana dalili hatari zifuatazo (yaani, mambo anayoyaona yeye mwenyewe):

Dalili hatari

  • Kutokuwa na hamu ya kula
  • Kutoongeza uzito
  • Udhaifu na magonjwa ya kimwili kwa ujumla
  • Vidonda, vipele, au matatizo mengine ya ngozi
  • Kidonda au kutokwa na damu kwa ufizi
  • Matatizo ya tumbo au kuhara
  • Joto au kufa ganzi miguuni.

Madhara ya upungufu wa madini ya iodini ni:

Mchoro 9.1 Tezi inaweza kuwa ishara ya hatari ya ukosefu wa madini ya iodini kwa chakula.
  • Tezi (uvimbe mbele ya shingo unaosababishwa na upungufu wa madini ya iodini; Mchoro 9.1)
  • Watoto wafupi
  • Watoto viziwi
  • Watoto walio na ukretini, ulemavu unao athiri fikira.

Kama unashuku kuwa afya ya mjamzito ni duni kutokana na lishe duni, au ukosefu wa virutubishi kwa mlo wake, mshauri kuhusu lishe bora na nyongeza ya iodini. Utajifunza jinsi ya kufanya hivi katika Kipindi cha 14 la Moduli hii.

Malengo ya Somo la Kipindi cha 9

9.2 Kuangalia uzito wake