9.3 Kuangalia joto lake

Joto la mwili ni kipimo cha jinsi tishu za ndani za mwili zilivyo moto au baridi. Ingawa inatofautiana kidogo wakati wa joto au baridi, au kama mtu amevaa nguo nyingi au chache mno, au anapofanya kazi nzito ya kimwili, inakaa kwa ujumla karibu na kiwango kinachojulikana kama joto ya 'kawaida', isipokuwa kama mtu ni mgonjwa. Joto la mwili hupimwa kwa kutumia chombo kitwacho kipimajoto (Kielelezo 9.2a), ambacho kina 'balbu' katika sehemu moja ya mwisho, kwa kawaida iliyojazwa na kiowevu cha chuma cha fedha inayoitwa zebaki. (Baadhi ya vipimajoto vilivyo vya glasi huwa na rangi nyekundu badala, na zingine hutumia teknolojia ya tarakimu. Angalia Kielelezo 9.2b) Katika kipimajoto cha glasi, wakatibalbu ya zebakiinapashwa joto na mwili wa mtu, zebaki inapanuka na kupanda hadi kwa tyubu nyembamba ya glasi, ambayo ina alama zilizo na nambari zinazoonyesha hali ya joto katika mwili wa mtu.

Kielelezo 9.2 (a) Kipimajoto cha glasi kinaweza kupima kwa Selisiasi(juu) au Farenhaiti (chini). (b) Kipimajoto cha tarakimukinachonyesha joto kama nambari iliyo kwa dirisha.

Joto la kawaida

Joto la kawaida ni karibu Nyuzi 37, au ni chini ya Farenhaiti 98. Hauhisi joto unapomgusa mama.

Ishara hatari

Mama ana joto jingi mwilini - joto zaidi ya Nyuzi 37.5 (au 100 Farenhaiti ). Unahisi joto unapomgusa mama.

Mchoro 9.3 Unaweza kuhisi kwa urahisi kama ni moto zaidi kukuliko.

9.2 Kuangalia uzito wake

9.3.1 Jinsi ya kupima joto lake