9.3.2 La kufanya iwapo mama ana joto jingi mwilini

Joto jingi mwilini inaweza kusababishwa na:

  • Ugonjwa - kwa mfano, homa au malaria
  • Maambukizi kwa sehemu ya mwili - kama vile maambukizi kwa kibofu cha mkojo, au uterasi
  • Joto kiasi pia inaweza kusababishwa na upungufu wa maji mwilini (upotezaji wa viowevu mwilini kutokana na kutokunywa maji ya kutosha).

Kama joto jingi mwilini halijashuka chini katika masaa nane, rufaa mama kwenye kituo cha afya.

Joto jingi mwilini inahitaji kupunguzwa mara moja. Ili kupunguza joto jingi mwilini:

  • Mpe paracetamol (miligramu) 500 - 1000 kwa kinywa kila baada ya saa 4-6
  • Anywe kikombe kimoja cha maji kila baada ya saa
  • Mwoshe mwili na kitambaa kilichowekwa katika maji baridi

9.3.1 Jinsi ya kupima joto lake

9.4 Kuchunguza mipigo yake kwa mshipa