9.6 Kuchunguza upungufu wa pumzi

Upumuaji wa kawaida

Baadhi ya upungufu wa pumzi, hasa wakati wa kipindi cha mwisho cha ujauzito, ni ya kawaida. Wanawake wengi hupata upungufu kiasi cha pumzi wakati wako na mimba ya miezi wa 8 au 9.

  • Je, unafikiri hii husababisha na nini?

  •  Mtoto anapokuwa mkubwa, anabana mapafu hivyo nafasi ya kupumua hupunguka. Upumuaji unaweza kuwa rahisi wakati mtoto anapoteremka chini katika tumbo muda mfupi kabla ya leba kuanza. 

    Mwisho wa jibu

Mchoro 9.8 Upungufu wa pumzi unaweza kuwa dalili ya hatari.

Dalili hatari

Kama upungufu wa pumzi unamfanya mjamzito kukosa utulivu, hii ni dalili hatari, hasa kama ana dalili zingine za ugonjwa (Mchoro 9.8).

Upungufu wa pumzi pia unaweza kusababishwa na:

  • Anemia
  • Matatizo ya moyo
  • Kifua kikuu
  • pumu
  • Maambukizi ya mapafu
  • Damu kuganda katika mapafu
  • Aleji.

Iwapo mjamzito ana matatizo ya kupumua wakati wote, au tatizo kali hata mara moja, au kama unashukuanaweza kuwa na ugonjwa wowote uliotajwa, mwelekeze kwenye kituo cha afya.

9.5 Kuchunguza dalili za anemia

9.7 Kuchunguza shinikizo lake la damu