9.7 Kuchunguza shinikizo lake la damu

Shinikizo la damu inamaanisha hali ambapo damu 'inasukuma' kuta za mishipa mikubwa ya damu inaposukumwa ndani ya mwili na moyo. Shinikizo la damu hupimwa kwa milimita ya zebaki (kiowevu cha chuma cha fedha, ambacho kina alama ya Hg ya kemikali), hivyo vipimo vya shinikizo la damu inaandikwa kama mmHg ikifuatiwa na nambari. Tutakuonyesha jinsi ya kupima shinikizo la damu katika Sehemu ya 9.7.1.

Madaktari na wauguzi huita nambari iliyo juu shinikizo la sistoli, na ya chini la diastoli.

Kipimo cha shinikizo la damu ni nambari mbili zilizoandikwa mmoja juu ya nyingine. Nambari iliyo juu itakueleza shinikizo la damu ya mama kwa wakati huyo moyo wake 'unapopiga' na kusukuma damu kwa mwili wake. Nambari ya chini itakueleza shinikizo la damu yake wakati moyo wake inapopumzika katikati ya mipigo, ili iweze kujaa damu tena.

Shinikizo la damu la kawaida

Shinikizo la damu la kawaida huwa kati ya mmHg 90/60 (useme hii kwa sauti ‘milimita tisini kwa sitini’ za zebaki,) na chini ya mmHg 140/90 (‘milimita mia moja arubanini kwa tisini’ za zebaki). Huwa haiongezeki sana wakati wa ujauzito.

Dalili za hatari

Shinikizo la juu la damu linajulikana kwa tiba kama hipatensheni na ni dalili ya hatari. Mama ana shinikizo la juu la damu ikiwa mmoja kati ya haya ni kweli:

  • Nambari ya juu ni 140 au zaidi.
  • Nambari ya chini ni 90 au zaidi.

Shinikizo la chini mno la damu (chini ya mmHg 90/50) pia ni daliliyahatari, ambayo kwa kawaida husababishwa tu na kuvuja kwingi kwa damu au mshtuko (upungufu hatari wa damu mwilini). Hali hii ni hatari sana.

Mama ambaye ana shinikizo la chini la damu anapaswa kupewa rufaa kwenye kituo cha afya kilichoko karibu mara moja.

Moyo ni kama pampu, inayosukuma damu mwilini. Shinikizo la juu la damu inamaanisha kwamba moyo lazima ifanye kazi kwa nguvu ili kusukuma damu kupitia mishipa zilizokazwa au nyweka (vena na ateri). Kiasi cha shinikizo la damu huonyesha ugumu ule damu inasukumwa. Kumbuka kwamba shinikizo la damu, si sawa na mpigo kwa mshipa. Unaweza kuwa na mpigo iliyo ya chini na shinikizo la juu la damu.

Ni muhimu sana kuchunguza shinikizo la damu ya mama kila anapotembelea kliniki ya wajawazito na kumpa rufaa kwenye kituo cha afya kama iko juu sana.

Wakati mama ana shinikizo la juu la damu wakati wa ujauzito, ni vigumu kwa damu yake kuleta chakula na oksijeni kwa mtoto kupitia plasenta. (Ulijifunza kuhusu haya katika Kipindi cha 5.) Kisha mtoto hukua polepole mno. Shinikizo la juu mno la damu linaweza pia kusababisha mama kuwa na matatizo ya figo, kuvuja damu kwa uterasi kabla ya kuzaa, au kuvuja damu kwa ubongo (kiharusi). Inaweza pia kuwa ni ishara ya prekilampsia, ambayo inaweza kusababisha kuzaa kabla ya wakati, kufuja damu, msukosuko, au hata kifo kwa mama.

9.6 Kuchunguza upungufu wa pumzi

9.7.1 Jinsi ya kupima shinikizo la damu