Malengo ya Somo la Kipindi cha 10

Baada ya kusoma katika kipindi hiki unapaswa uweze:

10.1 Kufafanua na kutumia kwa usahihi maneno yote muhimu yaliyochapishwa kwa herufi nzito. (Swali la Kujitathmini 10.1)

10.2 Kujua jinsi ya kupima urefu wa fandasi kwa kutumia mbinu ya vidole na chenezo laini. (Swali la Kujitathmini 10.1)

10.3 Kufasili vipimo vya urefu wa fandasi ili kukadiria ukuaji wa kawaida wa fetasi kulingana na umri wa ujauzito. (Swali la Kujitathmini 10.2)

10.4 Kutambua mambo yanayoweza kusababisha vipimo visivyo vya kawaida vya urefu wa fandasi na uchukue hatua mwafaka. (Swali la Kujitathmini 10.3)

Kipindi cha 10 Kukadiria Umri wa Ujauzito kutoka kwa Kipimo cha Urefu wa Fandasi

10.1 Je, kupima urefu wa uterasi ya mama hutueleza nini?