10.2 Jinsi ya kupima urefu wa fandasi

Ili kuhisi uterasi, mama anapaswa kulala chali na awe na viegemeo chini ya kichwa na magoti. Mweleze utakayofanya (na sababu ya kufanya hivyo) kabla ya kuanza kugusa fumbatio lake. Mguso wako unapaswa uwe thabiti lakini wa upole. Songesha vidole vyako kuelekea juu upande wa fumbatio (Mchoro 10.1) hadi utakapohisi sehemu ya juu ya fumbatio lake chini ya ngozi. Itahisika kama mpira mgumu. Unaweza kuhisi sehemu ya juu kwa kuzungusha vidole vyako pole pole kwenye fumbatio.

Mchoro 10.1 Mwanamke akiwa amelala chali, anza kwa kutafuta sehemu ya juu ya uterasi kwa vidole vyako. Kisha ujue mwanamke ana ujauzito wa miezi mingapi kwa kulinganisha idadi ya vidole na Mchoro 10.2 (kila mstari ni takriban upana wa vidole viwili).

10.1 Je, kupima urefu wa uterasi ya mama hutueleza nini?

10.2.1 Jinsi ya kupima urefu wa fandasi kwa mbinu ya kutumia vidole