10.2 Jinsi ya kupima urefu wa fandasi
Ili kuhisi uterasi, mama anapaswa kulala chali na awe na viegemeo chini ya kichwa na magoti. Mweleze utakayofanya (na sababu ya kufanya hivyo) kabla ya kuanza kugusa fumbatio lake. Mguso wako unapaswa uwe thabiti lakini wa upole. Songesha vidole vyako kuelekea juu upande wa fumbatio (Mchoro 10.1) hadi utakapohisi sehemu ya juu ya fumbatio lake chini ya ngozi. Itahisika kama mpira mgumu. Unaweza kuhisi sehemu ya juu kwa kuzungusha vidole vyako pole pole kwenye fumbatio.
10.1 Je, kupima urefu wa uterasi ya mama hutueleza nini?