10.2.1 Jinsi ya kupima urefu wa fandasi kwa mbinu ya kutumia vidole

Ikiwa sehemu ya juu ya uterasi iko chini ya kitovu, pima ni vidole vingapi vitakuwa chini ya kitovu. Ikiwa sehemu ya juu ya uterasi iko juu ya kitovu, pima ni vidole vingapi vitakuwa juu ya kitovu.

Mchoro 10.2 Kupima urefu wa fandasi kwa kutumia vidole. Mwanamke amelala chali. Kila mstari unawakilisha upana wa vidole viwili.
  • Tazama kwa makini Mchoro 10.2. Iwapo mtoto anakua kikawaida, je, uterasi inapaswa kuongezeka kwa upana wa vidole vingapi katika trimesta ya pili (miezi 3-6 ya ujauzito, au majuma 15-27 yaliyokamilika ya ujauzito)?

    Mchoro 10.3 Urefu wa fandasi baada ya miezi 7 ya ujauzito.
  • Urefu wa fandasi unapaswa kuongezeka kwa upana wa vidole 6 (upana wa vidole viwili kila mwezi) katika trimesta ya pili.

    Mwisho wa jibu

  • Je, ni upana wa vidole vingapi juu ya kitovu inapostahili kuwa sehemu ya juu ya uterasi baada ya miezi 7 ya ujauzito?

  • Tazama Mchoro 10.3 kupata jibu.

    Mwisho wa jibu

  • Je, utaelezaje mahali pa mstari wa nukta baada ya miezi 9 katika Mchoro 10.2 chini ya mstari unaoonyesha urefu wa fandasi baada ya miezi 8 ½ hadi 9?

  • Watoto wanaweza kuteremka chini majuma machache kabla ya kuzaliwa (tazama Kisanduku 10.1).

    Mwisho wa jibu

  • Tazama michoro katika Mchoro 10.4 (a) na (b). Je, ujauzito wa wanawake hawa ni wa majuma mangapi kwa mujibu wa mbinu ya kutumia vidole kupima urefu wa fandasi iliyoonyeshwa katika Mchoro 10.2?

    Mchoro 10.4 (a) na (b) Je, unafikiri michoro hii inaonyesha miezi mingapi ya ujauzito?
  • Katika Mchoro 10.4 (a) mwanamke ana takriban miezi 4 ½ ya ujauzito. Katika Mchoro 10.4 (b), yuko na takriban miezi 6 ½ ya ujauzito (vidole vitatu juu ya kitovu).

    Mwisho wa jibu

Unapopima urefu wa fandasi katika kila safari ya utunzaji katika ujauzito nakili idadi ya vidole ulivyotumia kupima urefu wa uterasi kwenye kadi yake. Weka alama ya ‘+’ (kuongeza) mbele ya nambari hiyo ikiwa sehemu ya juu ya uterasi iko juu ya kitovu. Weka alama ya ‘-’ (kutoa) mbele ya nambari hiyo ikiwa sehemu ya juu ya uterasi iko chini ya kitovu.

  • Je, ni vipi utakavyonakili vipimo vilivyoonyeshwa katika Picha 10.4 (a) na (b)?

  • Kipimo kilicho katika Mchoro 10.4 (a) kitaandikwa kama -2. Kipimo kilicho katika Mchoro 10.4 (b ) kitakuwa +3.

    Mwisho wa jibu

Upungufu wa mbinu ya kutumia vidole

Unapaswa kujua kuwa mbinu ya kutumia vidole kukadiria umri wa ujauzito (idadi ya majuma/miezi ya ujauzito) ina upungufu fulani unaoathiri usahihi wake.

  • Tazama mikono yako. Je, unaweza kusema ni kwa nini mbinu ya kutumia vidole inaweza kutoa makadirio tofauti ya umri wa ujauzito ikiwa wahudumu wa afya wawili tofauti walitumia mbinu hii kupima urefu wa fandasi ya mwanamke mmoja?

  • Kutokana na tofauti kubwa katika unene wa vidole vyetu, kunaweza kuwa na tofauti ya hadi majuma matatu kati ya kipimo cha urefu wa fandasi ya mwanamke mmoja kilichofanywa na watu wawili tofauti. (Hii huitwa ‘tofauti katika mitazamo ya wachunguzi,’yaani tofauti kati ya wachunguzi tofauti.)

    Mwisho wa jibu

Hata mhudumu mmoja akipima urefu wa fandasi ya mwanamke mmoja mara kadhaa kwa siku moja, huenda jibu likawa tofauti kila wakati kwa sababu mbinu ya kutumia vidole haina usahihi kamilifu. (Hii huitwa ‘tofauti katika mitazamo ya mchunguzi mmoja’, yaani tofauti kwa mchunguzi mmoja katika nyakati tofauti.)

Mwishowe, huenda umegundua kuwa umbali kati ya kinena simfisisi (mfupa wa kinena) na kitovu ni tofauti kati ya wanawake wakati hawana ujauzito na tofauti hii huathiri usahihi wa kipimo cha urefu wa fandasi kwa mbinu ya kutumia vidole. Kwa mfano, inachukulia kuwa umbali kati ya kinena simfisisi na kitovu ni sentimita 20 katika ujauzito wa majuma 20 bali inaweza kuwa ndefu sana hadi sentimita 30 na fupi sana hadi sentimita 14.

Kukabiliana na upungufu huu, imependekezwa kuwa upime urefu wa fandasi kwa chenezo laini iwapo unayo, jinsi ilivyoelezwa hapa chini.

10.2 Jinsi ya kupima urefu wa fandasi

10.2.2 Jinsi ya kupima urefu wa fandasi kwa chenezo laini