10.2.2 Jinsi ya kupima urefu wa fandasi kwa chenezo laini

Unaweza kutumia mbinu hii sehemu ya juu ya uterasi inapokua kufikia kitovu cha mwanamke.

Katika nusu ya pili ya ujauzito, ukubwa wa uterasi kwa sentimita huwa karibu na idadi ya majuma ambayo mwanamke amekuwa mjamzito. Kwa mfano, kama imekuwa majuma 24 tangu kipindi chake cha mwisho cha kawaida cha hedhi, urefu wa uterasi huwa sentimita 22-26. Uterasi inapaswa kukua kwa sentimita 1 kila juma, au sentimita 4 kila mwezi.

  1. Weka kitambaa au chenezo laini ya plastiki kwenye fumbatio la mama ukiwa umeshikilia alama ya 0 (sifuri) kwa chenezo hiyo kwenye sehemu ya juu ya mfupa wa kinena (tazama alama ya mshale katika Mchoro 10.5a).
  2. Fuata mkunjo wa fumbatio lake na ushikilie chenezo kwenye sehemu ya juu ya uterasi (Mchoro 10.5b).
  3. Andika idadi ya sentimita kutoka sehemu ya juu ya mfupa wa kinene hadi kwenye sehemu ya juu ya uterasi.
Mchoro 10.5 (a) Alama ya mshale imeelekezwa sehemu ya juu ya mfupa wa kinena. Weka alama ya 0 (sifuri) ya chenezo hapa. (b) Fuata mkunjo wa fumbatio la mwanamke na ushikilie chenezo kwenye sehemu ya juu ya uterasi.

Madaktari, wauguzi, na wakunga wengi hufundishwa kuhesabu muda wa ujauzito kwa majuma badala ya miezi. Wao huanza kuhesabu siku ya kwanza ya kipindi cha mwisho cha kawaida cha hedhi, ingawa mwanamke anaweza kuwa alipata ujauzito majuma mawili baadaye. Kuhesabu hivi hufanya ujauzito mwingi kuwa na muda wa majuma 40 (au unaweza kusema kuwa muda wa kawaida wa ujauzito ni majuma 40).

10.2.1 Jinsi ya kupima urefu wa fandasi kwa mbinu ya kutumia vidole

10.3 Je, na ikiwa ukubwa wa uterasi si ulivyotarajia?