10.3.1 Tarehe anayotarajiwa kuzaa uliyopata kwa kuhesabu tangu kipindi cha mwisho cha kawaida cha hedhi si sahihi

Kuna sababu kadhaa za uwezekano wa tarehe ya kutarajia kuzaa tangu kipindi cha mwisho cha kawaida cha hedhi kutokuwa sahihi. Wakati mwingine wanawake hawakumbuki tarehe ya kipindi chao cha mwisho cha kawaida cha hedhi kikamilifu. Wakati mwingine mwanamke hukosa hedhi kwa sababu nyingine, na kisha apate ujauzito baadaye. Mwanamke huyu anaweza kuwa na ujauzito mchanga kuliko ulivyofikiria na kwa hivyo uterasi ni ndogo kuliko unavyotarajia. Au wakati mwingine mwanamke anatokwa na damu kidogo baada ya kupata ujauzito. Iwapo alichukulia kuwa hiyo ilikuwa kipindi chake cha mwisho cha kawaida cha hedhi, mwanamke huyu atakuwa na ujauzito wa mwezi moja au miwili zaidi ya ulivyofikiria. Uterasi itakuwa kubwa kuliko unavyotarajia.

Kumbuka kuwa tarehe za kutarajiwa kuzaa si kamili kabisa. Mara nyingi wanawake huzaa hadi baada ya au kabla ya majuma mawili au matatu kutoka tarehe wanayotarajiwa kuzaa. Hii huwa salama.

Ikiwa tarehe ya kutarajia kuzaa hailingani na ukubwa wa uterasi katika safari ya kwanza, nakili. Subiri na upime tena uterasi baada ya kati ya majuma mawili au manne. Iwapo uterasi itakua kwa takriban upana wa vidole viwili au sentimita 1 kwa mwezi, tarehe ya kutarajia kuzaa uliyopata kwa kuhisi sehemu ya juu ya uterasi inaweza kuwa si sahihi. Huenda tarehe ya kutarajia kuzaa uliyopata kutoka kwa kipindi cha mwisho cha kawaida cha hedhi si sahihi.

10.3 Je, na ikiwa ukubwa wa uterasi si ulivyotarajia?

10.3.2 Uterasi inakua haraka sana