10.3.2 Uterasi inakua haraka sana

Ikiwa uterasi inakua zaidi ya upana wa vidole viwili kwa mwezi, au zaidi ya sentimita 1 kwa juma, kuna uwezekano wa visababishi kadhaa tofauti:

  • Huenda mama ana pacha.
  • Huenda mama ana kisukari melitasi.
  • Huenda mama ana maji mengi (kiowevu cha amnioni) kwenye uterasi.
  • Huenda mama ana ujauzito bandia (tyuma badala ya mtoto).

Ukifikiri kuwa huenda kukawa na pacha, hata ikiwa kuna mpigo mmoja tu wa moyo, mpe mwanamke huyo rufaa aende katika kituo cha afya kilicho karibu.

Huenda mama ana pacha

Inaweza kuwa vigumu kujua kwa hakika kuwa mama ana ujauzito wa pacha.

Ishara za pacha ni:

  • Uterasi hukua haraka au huwa kubwa zaidi ya kawaida.
  • Unaposhika fumbatio la mama, unaweza kuhisi vichwa viwili au matako.
  • Unaweza kusikia mipigo miwili ya moyo. Hii si rahisi kutambua, lakini inaweza kutambulika katika miezi miwili ya mwisho.

Tutakuonyesha jinsi ya kusikiza mpigo wa moyo wa fetasi kupitia kwa fumbatio la mama katika Kipindi cha 11. Kwa sasa, tunalenga pacha kama kisababishi cha uterasi kuwa kubwa zaidi ya inavyotarajiwa. Hapa kunazo njia mbili za kusikiza mipigo ya mioyo ya pacha:

Mchoro 10.6 kupiga kwa mioyo ya fetasi kwa mwendo sawa kunaweza kukuonyesha ikiwa mtoto ni mmoja au wawili.
  1. Tafuta mpigo wa moyo wa mtoto mmoja. Mwambie msaidizi asikize sehemu zingine ambako mpigo wa moyo ni rahisi kusikika. Akisikia mpigo wa moyo, mwambie asikize sehemu moja huku nawe ukisikiza sehemu nyingine. Kila mmoja wenu anaweza kutumia mkono wake kupiga mpigo wa moyo. Ikiwa midundo ni sawa, huenda mnasikiza mtoto mmoja. Ikiwa mipigo si sawa, huenda mnawasikiza watoto wawili tofauti (Mchoro 10.6).
  2. Ikiwa huna msaidizi, bali una saa iliyo na mshale wa sekunde au kipima saa cha kujitengenezea, jaribu kupima kila mpigo wa moyo kivyake. Ikiwa mipigo hiyo ya moyo si sawa, huenda unasikiza watoto wawili tofauti.

Kwa kuwa uzazi wa pacha ni mgumu au hatari kuliko ule wa mtoto mmoja, ni salama kwa mwanamke kwenda hospitalini kwa kuzaa. Kwa kuwa pacha wana uwezekano mkubwa wa kuzaliwa mapema, mama anafaa kuwa na usafiri tayari wakati wote baada ya mwezi wa sita wa ujauzito. Ikiwa hospitali iko mbali sana, ni vyema mama kusonga karibu katika miezi ya mwisho ya ujauzito. Hakikisha una mpango wa jinsi ya kupata usaidizi wakati wa dharura.

Huenda mama ana kisukari melitasi

Ulijifunza kuhusu ishara za hatari za kisukari katika Kipindi cha 9.

  • Je, ni nini utakachotarajia kupata iwapo mwanamke ana ishara zote za hatari za kisukari?

  • Mpe mwanamke huyo rufaa aende katika kituo cha afya ukishuku kuwa huenda ana kisukari melitasi.

    Alikuwa na kisukari katika ujauzito uliopita. Mmoja wa watoto wake wa hapo awali alizaliwa akiwa mkubwa sana (zaidi ya kilo 4), au alikuwa mgonjwa au alifariki akizaliwa na hakuna anayejua sababu. Ni mnene. Anahisi kiu kila wakati. Anajikuna mara kwa mara na harufu mbaya kutoka ukeni mwake. Vidonda vyake vinapona pole pole. Anakojoa mara kwa mara zaidi ya wanawake wengine wajawazito. Uterasi yake ni kubwa zaidi ya kawaida kulingana na umri wa ujauzito. Unapofanya uchunguzi wa dipstick, kuna sukari kwenye mkojo wake (Sehemu ya 9.8.1 ya Kipindi cha 9).

    Mwisho wa jibu

Maji mengi sana kwenye uterasi

Maji mengi sana (kiowevu cha amnioni) si tatizo wakati wote, bali yanaweza kufanya uterasi kutanuka sana. Kisha uterasi haiwezi kunywea ipasavyo ili kusukuma mtoto nje, au kuzuia kutoka kwa damu baada ya kuzaa. Katika hali chache mno inaweza kumaanisha kuwa mtoto atakuwa na matatizo ya kuzaliwa. Jaribu kumpa mwanamke huyu rufaa aende katika kituo cha afya kinachoweza kumpa sonogramu (uchunguzi wa mawimbi ya vijisauti) ikiwa kipimo cha uterasi ni kikubwa sana na hutarajii pacha.

Ujauzito bandia (tyuma)

Wakati mwingine mwanamke hupata ujauzito, bali tyuma hukua badala ya mtoto. Hii huitwa ujauzito bandia (Mchoro 10.7). Madoadoa ya damu na tishu (wakati mwingine zenye umbo la zabibu) vinaweza kutoka ukeni mwake.

Mchoro 10.7 Ujauzito bandia (tyuma) ukikua kwenye uterasi badala ya mtoto.

Ukitambua ishara na dalili za ujauzito bandia, mpe mwanamke huyo rufaa aende hospitalini haraka iwezekanavyo. Tyuma hiyo inaweza kuwa saratani na kumwua, wakati mwingine haraka sana. Daktari wa upasuaji anaweza kuondoa tyuma hiyo ili kuokoa maisha ya mwanamke huyo.

Dalili zingine za ujauzito bandia ni:

  • Mpigo wa moyo wa fetasi hausikiki.
  • Mtoto hawezi kuhisika.
  • Mwanamke amekuwa na kichefuchefu muda wote katika ujauzito.
  • Ana madoadoa ya damu, na tishu zenye umbo sawa na mkungu wa zabibu kutoka ukeni.

10.3.1 Tarehe anayotarajiwa kuzaa uliyopata kwa kuhesabu tangu kipindi cha mwisho cha kawaida cha hedhi si sahihi

10.3.3 Uterasi inakua polepole sana