Maswali ya kujitathmini ya Kipindi cha 10

Kwa kuwa umekamilisha kipindi hiki, unaweza kutathmini ni kwa kiasi kipi umeweza kutimiza Malengo yake kwa kujibu maswali yanayofuata uchunguzi maalum 10.1. Andika majibu yako kwenye Shajara yako ya Masomo na ujadili na mkufunzi wako katika mkutano saidizi wa masomo utakaofuata. Unaweza kulinganisha majibu yako na muhtasari juu ya Maswali ya Kujitathmini mwishoni mwa Moduli hii.

Uchunguzi Maalum 10.1 Abebech

Abebech ni mwanamke mjamzito ambaye umri wa ujauzito wake ni miezi sita kulingana na kipindi chake cha mwisho cha kawaida cha hedhi. Unapomchunguza, unaweza kuhisi kuwa fandasi yake iko upana wa vidole vinne juu ya kitovu chake na unaweza kuusikia mpigo wa moyo vizuri.

Swali la Kujitathmini 10.1 (linatathmini Malengo ya Somo 10.1 na 10.2)

  • a.Je, umri wa ujauzito wa Abebech ukitumia kipimo cha urefu wa fandasi ni upi?
  • b.Je, fumbatio la Abebech lingekuwa sentimita ngapi kutoka kwa mfupa wa kinena hadi juu ya uterasi yake ili kuthibitisha kipimo chako cha urefu wa fetasi?

Answer

  • a.Umri wa ujauzito huu kulingana na kipimo cha urefu wa fandasi ni miezi saba.
  • b.Ikiwa kweli Abebech ni mjamzito wa miezi saba, utatarajia fumbatio lake kuwa sentimita 28 kutoka kwa mfupa wa kinena hadi juu ya uterasi, yaani, takribani sentimita 1 kwa kila juma la ujauzito tangu kipindi chake cha mwisho cha kawaida cha hedhi. Kumbuka kuwa kipimo kinaweza kuwa kati ya sentimita 26 na 30.

Mwisho wa jibu

Swali la Kujitathmini 10.2 (linatathmini Lengo la Somo 10.3)

Je, umri wa ujauzito wa Abebech kulingana na kipimo cha urefu wa fandasi unalingana na umri wa ujauzito huo uliokokotolewa tangu kipindi chake cha mwisho cha kawaida cha hedhi?

Answer

Umri wa ujauzito kulingana na urefu wa fandasi ni mwezi mmoja zaidi ya inavyotarajiwa tangu tarehe ya kipindi cha mwisho cha kawaida cha hedhi. Kwa hivyo, uterasi ni kubwa zaidi ya inavyotarajiwa tangu tarehe ya kipindi cha mwisho cha kawaida cha hedhi.

Mwisho wa jibu

Swali la Kujitathmini 10.3 (linathmini Lengo la Somo 10.4)

Je, ni maelezo yapi unayoweza kutoa kwa matokeo yako katika kisa cha Abebech, na ni hatua zipi utakazochukua?

Answer

Huenda uterasi ni kubwa zaidi ya inavyotarajiwa kwa sababu tarehe ya kipindi chake cha mwisho cha kawaida cha hedhi inaweza kuwa si sahihi, na kwa hakika Abebech ana ujauzito wa miezi saba. Hili si tatizo, lakini ni muhimu kuchunguza maelezo mengine yoyote. Kwa mfano, huenda ana kiowevu kingi cha amnioni (maji) kinachomzunguka mtoto kwenye uterasi; mpe rufaa aende kwenye kituo cha afya kwa uchunguzi wa mawimbi vijisauti kujua iwapo hili ndilo tatizo. Au huenda ana ujauzito wa pacha. Unaweza kusikia vizuri mpigo mmoja wa moyo wa fetasi, kwa hivyo tafuta mtu mwingine akusaidie kusikiza kwenye fumbatio la Abebech ili kuona ikiwa mtasikia mipigo miwili ya mioyo ya fetasi. Ukishuku kuwa ana pacha, mpe rufaa aende kwenye kituo cha afya kilicho karibu.

Mwisho wa jibu.

Muhtasari wa Kipindi cha 10