Malengo ya Somo la Kipindi cha 11

Baada ya kipindi hiki, unapaswa uweze:

11.1 Kufafanua na kutumia kwa usahihi maneno yote muhimu yaliyochapishwa kwa herufi nzito. (Swali la kujitathmini 11.1)

11.2 Kujua jinsi ya kutambua mkao wa kawaida na usio wa kawaida kwa utomasaji na oskalitesheni. (Maswali ya kujitathmini 11.1 na 11.2)

11.3 Kujua jinsi ya kutathmini hali njema ya fetasi kwa oskalitesheni na kucheza kwa fetasi. (Maswali ya kujitathmini 11.1, 11.3 na 11.4)

11.4 Kutambua hali za fetasi zinazohitaji kupewa rufaa kwenda katika kituo cha afya kilicho karibu. (Swali la kujitathmini 11.4)

Kipindi cha 11 Kutathmini Fetasi

11.1 Kujua mkao wa mtoto kwenye uterasi